Header Ads Widget

MIKOPO YA VIKUNDI HALMASHAURI YADAIWA KUNA UBADHILIFU

Mbunge wa Ulyankulu, Rehema Migila akichangia bungeni kuhusu jinsi mikopo ya vikundi katika halmashauri inavyotumika vibaya, Picha na Edwin Mjwahuzi

Ni kilio cha ubadhirifu wa fedha za mikopo inayotolewa na halmashauri kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu katika maeneo mengi ya nchi.

Wakati wabunge wakipigia kelele ubadhirifu wa fedha hizo zilizokusudiwa zirejeshwe ili zisaidie watu wengine, wadau wameshauri sekta binafsi ihusishwe katika kamati za mikopo na utoaji elimu ya biashara ili kuondokana na tatizo hilo.

Juzi Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), David Silinde alikiri kuwepo kwa ubadhirifu katika mikopo hiyo, akasema wanakusudia kubadili sheria na kanuni za mikopo hiyo inayotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri.
 
SOMA ZAIDI HAPA; CHANZO MWANANCHI.

Post a Comment

0 Comments