Header Ads Widget

WATU WANNE WAFARIKI DUNIA WAKICHIMBA KABURI, WENGINE WAJERUHIWA

Watu wanne wamefariki dunia papo hapo na mwingine kujeruhiwa baada ya kupigwa na radi wakati wakichimba kaburi katika Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya.

Watu hao walipigwa na radi Jumapili Januari 9, 2022 wakichimba kaburi kwa ajili ya kumzika ndugu yao aliyefariki Januari 7.

Mkuu wa Wilaya ya Chunya (DC), Mayeka Mayeka amethibitisha kutokea tukio hilo huku akiwataja waliofariki kuwa ni pamoja na Yohana James (30), Paul Mwasongole (40), Swalehe Ibrahim (23) wakazi wa Chunya mjini na Bonny Lauliano mkazi Mkoa wa Songwe.

SOMA ZAIDI HAPA   CHANZO MWANANCHI

 

Post a Comment

0 Comments