Header Ads Widget

WAWILI WAFIKISHWA MAHAKAMA YA KISUTU KWA KUMDANGANYA DPP KUWA NI MAAFISA USALAMA WA TAIFA

Mwonekano wa Mbele wa Jengo la Mahakama ya  Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam 

Na Rebeca Kwandu Dar es Salaam.

 Mfanyabiashara, Joshua Jelemia (37) na Yahaya Abdallah (31) wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam  kujibu mashtaka mawili ya kujifanya Maofisa Usalama wa Taifa (TISS) katika ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP) na naibu mkurugenzi wa mashtaka.

 Washtakiwa hao wamefikishwa katika Mahakama hiyo Juni 18, 2021 na kusomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi,  Godfrey Isaya. 

Wakiwasomewa Mashtaka na  wakili wa Serikali Mwandamizi,  Wankyo Simon amedai  kuwa watuhumiwa hao walitenda  makosa hayo Juni 12, 2021  katika ofisi za DPP zilizopo jengo la Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 

 Inadaiwa siku hiyo wawili hao walifika Ofisini kwa (DPP) Slyvester Mwakitalu  na naibu wake (DDPP), Joseph Pande na kujitambulisha   kuwa wao ni maofisa kutoka TISS.

 Baada ya kusomewa Mashitaka hayo, upande wa Mashtaka umedai upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na hivyo wapangiwe tarehe nyingine kwa ajili ya  kuwasomea washtakiwa hoja za awali. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Juni 22, 2021 na washtakiwa kurudishwa rumande baada ya kukosa dhamana.

Post a Comment

0 Comments