Header Ads Widget

WAKAZI ZAIDI YA ELFU 14 MWAKITOLYO KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI YA ZIWA VICTORIA



Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mh Jasinta Mboneko akisikiliza maelezo toka kwa Mkurugenzi wa Kashwasa Muhandisi Joshua Mgeyekwa juu ya utekelezaji wa mradi huo wa maji toka Solwa hadi mwakitolyo.

Wakazi zaidi ya elfu kumi na Nne wa Kata ya  Mwakitolyo halmashauri ya wilaya ya Shinyanga wanatarajia kuondokana na adha ya upatikanaji wa maji baada ya mradi mkubwa wa maji toka ziwa kuanza kutekelezwa chini ya mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Kahama Shinyanga Kashwasa.

Akizungumzia utekelezaji wa mradi huo Mkurugenzi wa  Kashwasa Muhandisi Joshua Mgeyekwa amesema kuwa zoezi linaloendelea kwa sasa ni ulazaji wa mabomba ya chuma ambayo yatapeleka maji kwenye tanki kubwa lilioko Mwakitolyo ili kuwezesha utoaji wa huduma ya maji kwa wananchi.

 Muhandisi Mugeyekwa amesema kuwa mradi huo umepitiwa na kufanyiwa  upya usanifu kwa ushirikiano kati ya Ruwasa na Kashwasa  baada ya mradi wa awali uliokuwa ukisimamiwa na halmashauri ya wilaya ya shinyanga kushindwa kufikisha maji kama ilivyokusudiwa.

“Baada ya usanifu tumeweza kubadilisha  aina ya mabomba kwa kutoa ya  awali mabayo yalikuwa ya Plastiki na  kuweka mabomba ya chuma yenye uwezo wa kuimili msukumo mkubwa  wa maji yaani (Presha ya maji) inyaofikia zaidi ya Mita 400 PN 40 ambapo tunachukilia maji pale Solwa na kupeleka kwenye tanki ambalo tayari lilishajengwa awali lenye ujazo wa Mita 90 na  urefu wa hili bomba ni  Kilomita 20.6”

Mugeyekwa amesema kuwa tayari wamepokea mabomba yenye kufikia kilomita 14 ambapo wanasubiria bomba zilizosalia pamoja na vifaa vya kuungia huku akibainisha kuwa mradi huo utakapokamilika utahudumia wakazi wa mwakitolyo, mawemiru na sehemu za jirani kwa wananchi wapatao  elfu  kumi nne na mia sita(14600)

“Mpaka sasa hivi ujenzi umefikia asilimia 60 na tulitegemea  tujenge mradi huu kwa siku 90 yaani miezi mitatu lakini sasa hivi  tumetumia siku 45 lakini ndani ya mwezi mmoja au zaidi tutakuwa tumemaliza”

William Msabi  ni fundi sanifu kutoka kashwasa  amesema kuwa zoezi la uchimbaji wa mtaro  huo lilianza tarehe 16 mwezi wa sita na tarkibani kilmita 17 zimechimbwa  huku kilomita 14 zikiwa tayari zimelazwa bomba huku akieleza kuwa katika utekelezaji wa mradi huo wamekumbana na changamoto mbalimbali ikiwemo miamba pamoja na udongo ambao umekuwa ukiwatatiza.

Kwa upande  wake  mkuu wa wilaya ya Shinyanga amesema kuwa miradi mingi ya maji  inayotekelezwa na wakandarasi imekuwa ikisua sua  pamoja na kuchukua muda mrefu na kushindwa kutoa huduma kwa jamii kwa wakati.

Matumaini  makubwa  ya wananchi wa kata ya  mwakitolyo ni kuona kuwa wanapata maji na ndicho kilio chao kikubwa  kwa hiyo nami nimekuja kujionea kwamba kazi hii ipo kwenye hatua gani ukizingatia kwamba eneo hili lina changamoto kubwa ya maji hasa ukianzia mwezi wa 12 hadi wa  4 kulikuwa kumejaa maji hapa na kushindwa kutekelezeka kwa mardi hata wananchi walikuwa wakisafiri kwa mitumbi hata barabara zilikuwa zimekatika”

Mboneko amesema kuwa serikali  kupitia kwa waziri wa Maji Profesa Makame Mbarawa imehaidi kuleta fedha kwa ajili ya kumalizia mradi huo na kusema kuwa mategemeo makubwa ni kukakamilika kabla ya mvua kuanza kunyesha ili wakazi wa Mwakitolyo waweze.

Niwapongeze wananchi na wakazi wote wa Mwakitolyo  na kata jirani kwa kuendelea kutunza miundombinu hii ya maji kulinda mabomba haya pia kufanya kazi ya kuchimba mitaro kwa kweli ninawashukuru sana waendelee kutoa ushirikiano na kulinda na kutunza miundombinu hii”

Mradi huo unatekelezwa na Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Kahama Shinyanga (KASHWASA) na Wakala wa maji vijijini(RUWASA)  kwa gharama ya shilingi bilioni 2 milioni 298 na laki 7 na elfu 51  mia 343 (2.398,751,343)  ambapo awali uligharimu shilingi bilioni 1.4.

 Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya ya Shinyanga wakiendelea kukagua  na kuangalia  maungio ya maji eneo la solwa ambapo 
 Wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama viongozi wa kashwasa na ruwasa wakitembelea eneo ambalo mradi wa maji utaanzia kuelekea mwakitolyo.

 wajumbe wa kamati ya ulinzi,watendaji wa kashwasa na ruwasa wakiangalia namna ambavyo mabomba ya chuma yanavyounganishwa chini ni mafundi wa mabomba kutoka kashwasa pamoja na wananchi wakishirikiana kulaza mabomba
 Shughuli za kuunganisha Mabomba zikiendelea eneo la Mwakitolyo
 Zoezi la kulaza mabomba linaendelea ili kuhakikisha wakazi wa Mwakitolyo wanapata huduma ya maji safi na salama
 Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Kashwasa Muhandisi Joshua Mgeyekwa akifuatiwa na mkuu wa wilaya ya Shinyanga wakiteta jambo wakati zoezi la ulazaji na uunganishaji wa mabomba ukiendelea.

 Mafundi wakiendelea na zoezi la kuunganisha mabomba ya chuma.
 
  Hili ni eneo la Mwakitolyo  ambalo huwa linajaa maji wakati wa msimu wa mvua  kwa mbali ni mwoneko wa njia ya bomba la maji linaloendelea kulazwa.
  Wajumbe wakiendelea na kukagua mradi huo unaotekelezwa na Kashwasa kwa ushirikiano na Ruwasa 
 zoezi la kuunganisha  mabomba likiendelea chini ya usimamizi wa mafundi toka kashwasa pamoja na wananchi ili kusogeza huduma ya Maji karibu ikiwa ni mwelekeo wa serikali wa kumtua ndoo mwanamke.
baadhi ya Mabomba yakiwa eneo la kuunganishwa 
Tayari mabomba yameunganishwa na kulazwa ndani ya mtaro yakisubiri kufukiwa