Header Ads Widget

DC MBONEKO ATEMBELEA MGODI WA ZEM DEVELOPMENT MWAKITOLYO AWATAKA KUTEKELEZA MAKUBALIANO YA MKATABA WAO

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akitoa maelekezo kwa uongozi wa Mgodi wa ZEM uliopo eneo la Mahiga kata ya Mwakitolyo wilayani Shinyanga.
Kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Shinyanga ikiwa chini ya duara lililojengwa kisasa zaidi wakikagua maendeleo  ya mradi huo eneo la Mahiga Kata ya Mwakitolyo.

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mh Jasinta Mboneko  ametembelea na kukagua Mradi wa  Uchimbaji wa Madini aina ya Dhahabu eneo la Mahiga Kata ya Mwakitolyo ambapo amtembela maduara  ya  kisasa yatakayotumika kwa shughuli mbalimbali ikiwemo kuingiza magari kwa ajili kutolea mawe pamoja na kuingiza hewa safi kwenye mashimo hayo.

Mradi huo  unaotekelezwa na kampuni ya ZEM Development ya Nchini Uchina Katika eneo la Mwakitolyo halmashauri ya Wilaya  ya Shinyanga.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo Ramadhan Bunyese ambaye ni  Mlipuaji wa Miamba katika eneo hilo amesema kuwa kwa sasa wako katika uchorongaji wa Miamba ili kufanya uchimbaji kuwa rahisi.

“Uchimbaji huu tunaufanya kutoka juu hadi chini tunatarajia kwenda umbali wa  mita mia moja na hamsini kutoka juu hadi chini  ya ardhi kisha tutaziunganisha ili kuwezesha mawasiliano kwa pamoja hivyo tunajitahidi kwenda kwa kasi ili mwezi wa Sita Mwakani tuanze uzalishaji”  amesema Ramadhan

Muhandisi wa Madini toka ofisi ya madini Mkoani Shinyanga Gilliard Luyoka amesema kuwa uchimbaji huo umefuata hatua zote za serikali,  ikiwemo utoaji wa vibari kwa kila hatua wanayofikia ikiwemo ukaguzi wa idara ya mazingira toka ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira NEMC sambamba na ujengwaji wa Bwawa litakalotumika kumwaga taka zitakazotoka kwenye processing Plant.

Kwa upande wake Meneja Miradi wa ZEM DEVELOPMENT Kevin Wang amebainisha kuwa kutokana na makubaliano yao   kabla ya kuanza utekelezaji wa mradi huo ilikuwa ni kushiriki kuchangia shughuli za maendeleo ndani ya kijiji na Kata ya Mwakitolyo hususani katika Sekta ya elimu, afya n.k ambapo tayari wamekwisha changia ujenzi wa jengo la serikali ya kijiji.

“Ni Jukumu letu kuwajibika kwa Jamii kwa kuchangia shughuli za maendeleo ambapo tayari mwaka jana tumechangia ujenzi wa  ofisi ya kijiji na mwakani tunajenga Jengo la huduma za Nje OPD katika Zahanati ya mwakitolyo”

Wang  ameongeza kuwa katika makubaliano yao  ni pamoja na kujenga shule ya Msingi,huduma za kijamii ambapo wamehaidi kushiriki moja kwa moja ambapo wamehaidi pia kuchangia miradi  mbalimbali ya maendeleo .

"Tuko mbioni kuonana  na uongozi wa Wilaya chini cha Mkuu wa Wilaya pamoja na Mkurugenzi ili kuelezea mambo muhimu ya maendeleo"

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Bi Jasinta Mboneko ameutaka uongozi wa mgodi huo kuanza uchangiaji wa shughuli za maendeleo eneo hilo la Mwakitolyo na kwa serikali kwa ujumla ambapo awali walibainisha baada ya   eneo hilo kupatikana wataanza kulipa kodi ya halmashauri ambayo wamewatakiwa  kuanza kulipa.

“Hii ni sehemu ya makubaliano katika Mkataba wenu hivyo lazima muanze kulipa halmashauri ili iweze kupata fedha toka kwenu hapa, lakini pia kwa sababu mnaishi na jamii kuna vitu viko kwenye makubaliano ikiwemo ujenzi wa Shule,Hospital na hata ulinzi hivyo lazima mshiriki kwenye shughuli hizi siyo kungoja muanze uzalishaji mwakani”

Mboneko ameongeza kuwa kutokana na idadi kubwa ya wakazi wa Mwakitolyo kutokana na shughuli zinazoendelea  lazima kuwepo kwa kituo cha polisi ambacho kitasaidia kuimarisha ulinzi na usalama na  kuwataka wadau wote wa maendeleo wakiwemo wachimbaji, blockers na mgodi huo wa ZEM kuchangia ili kurahisha upatikanaji wa fedha zitakaoendeleza jengo ambalo limeishia kwenye msingi.

“Nakuagiza afisa mtendaji wa kata  hii ya Mwakitolyo (WEO) kuhakikisha kuwa ifikapo mwishoni mwa mwezi huu August 30 wadau wote wawe wamechangia ili tuweze kujenga  kituo cha polisi ili kuimarisha ulinzi wenu hapa”

Mboneko ametembelea na kukagua maeneo  pamoja na Blockers waliopo mwakitolyo huku akizungumza na wachimbaji wadogo, blockers pamoja viongozi wa mgodi wa ZEM uliopo eneo la Mahiga.

Meneja Miradi wa ZEM Development Bw Kevin Wang akiongea na  kamati ya usalama na ulinzi ikiongozwa na mkuu wa wilaya hiyo Jasinta Mboneoko

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta mboneko akiteta jambo juu ya uhifadhi wa Mazingira 
  
 Mojawapo ya Maduara ya Kisasa ya uchimbaji wa Madini ya Dhahadu katika Mgodi wa ZEM uliopo Mahiga Mwakitolyo 

Gilliard Luyoka muhandisi wa madini  toka ofisi ya madini akitoa maelezo ya namna wanavyosimamia sheria za madini
 Mkuu wa wilaya ,kamati ya ulinzi na usalama pamoja na uongozi wa mgodi wa Zem wakikagua maeneo mbalimbali ya mgodi huo.

 Mlango wa kuingia kwenye moja ya maduara ya Zem Mahiga Mwakitolyo 

 Baadhi ya wafanya kazi wa Mgodi wa ZEM wakiendelea na kazi 

Tazama picha mbalimbali za Matukio ya ziara ya kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Shinyanga ikongozwa na mkuu wa wilaya hiyo Jasinta Mboneko katika eneo la Mwakitolyo




  
  
  








   
  

  



 Mkuu wa Polisi wilaya yShinyanga (OCD) Kafumu Lutonjaa