Header Ads Widget

WATOTO ZAIDI YA 300 WANAOISHI MAZINGIRA MAGUMU WAPATA TUMAINI LA ELIMU


Moja ya madarasa yanayojengwa kupitia juhudi za wadau mbalimbali wakiwemo waimbaji wa nyimbo za injili ili kuwasaidia watoto walio katika mazingira magumu kupata elimu.

Na Mwandishi Wetu - Shinyanga Press Club Blog
WATOTO zaidi ya 300 wanaoishi katika mazingira magumu wakiwamo yatima na walemavu katika kata ya kagongwa wilayani kahama wameokolewa katika wimbi la kukosa elimu kwa kujengewa madarasa ya kusomea na wadau wa elimu wa eneo hilo la kagongwa lengo likiwa ni kuhakikisha watoto hao waliokosa elimu ya awali wanapata elimu kama ilivyo kwa watoto wengine nchini.

Majengo hayo ya madarasa yamejengwa kwa ushirikiano wa waimbaji wa nyimbo za injili na wadau mbalimbali wakiwemo waimbaji wa nyimbo za injili, Bahati Bukuku na Saulo Maziku ambao wamejitolea mauzo ya albamu zao zinazouzwa yaende kujenga shule kwa ajili ya watoto wenye mahitaji.

Baadhi ya wanafunzi kutoka kwenye makundi hayo akiwemo Elizabeth Ernest wameonyesha faraja yao na kuwashukuru wadau, huku mlezi wao Mchungaji Samwel Bundala aliomba msaada zaidi wa wadau kuendelea kusaidia makundi hayo.

Kwa upande wake mwakilishi wa mkuu wa wilaya ya Kahama, Jerome Lugome ambaye ni Afisa Mtendaji Kata ya Kagongwa wilayani Kahama amesema serikali imeendelea kujali michango ya wadau katika kuendeleza sekta ya elimu huku akitoa wito kwa wadau wengine kujitokeza kuhakikisha watoto hao wanapata haki ya elimu na mahitaji mbalimbali.
 Waimbaji wa nyimbo za injili, Saulo Maziku na Bahati Bukuku ambao walihudhuria zoezi hilo
Mchungaji na Mlezi wa watoto hao, Samwel Bundala
Bahati Bukuku
 Baadhi ya wananchi waliohudhuria zoezi hilo
 Mmoja wa wanafunzi hayo, Elizabeth Ernest
 Zoezi la uuzaji Albamu kutoka kwa waimbaji wa injili likiendelea
 Baadhi ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu katika kata ya Kagongwa wilayani Kahama
Mwimbaji wa nyimbo za Injli, Bahati Bukuku

 Zoezi likiendelea
Waimbaji wa nyimbo za injili akiwemo Bahati Bukuku (kulia) akishiriki kuuza albamu ambazo mapato yake yatasaidia watoto walio katika mazingira magumu
Wadau mbalimbali waliojitokeza kushiriki katika zoezi hilo.