Header Ads Widget

HII NDIYO DAWA ANAYOTUMIA RAIS TRUMP KUJIKINGA NA CORONA


Rais wa Marekani Donald Trump amesema kwamba anakunywa dawa ya hydroxychloroquine kujikinga dhidi ya virusi vya corona hata ingawa maafisa wa afya wametoa onyo juu ya usalama wa dawa hiyo.

Akizungumza katika Ikulu ya White House, aliwaambia wanahabari kwamba ameanza kunywa dawa hizo zinazotibu ugonjwa wa malaria na hivi karibuni imetumika kutibu ugonjwa wa ngozi.

"Nimekuwa nikiinywa kwa karibia wiki moja na nusu sasa na niko hapa, bado niko hapa," hilo lilikuwa tangazo lake la kushangaza.

Hakuna ushahidi unaoonesha kwamba dawa ya hydroxychloroquine ina uwezo wa kukabilina na virusi vya corona na wataalamu wanaonya kuwa inaweza kusababisha matatizo ya moyo.
Trump amesema nini?

Rais huyo, mwenye miaka 73, alikuwa ameitisha mkutano kwa ajili ya kuzungumzia sekta ya migahawa Jumatatu, aliposhutukiza wanahabari kwa kuwafahamisha kwamba amekuwa akinywa dawa hiyo.

"Utashangaa ni watu wangapi wanaokunywa dawa hii, hasa wafanyakazi waliomstari wa mbele katika kukabiliana na janga la virusi vya corona kabla ya wewe kuipata, wahudumu wa afya, wengi wao tu wanakunywa dawa hii," aliwaambia wanahabari. "Mimi pia ninainywa."

Alipoulizwa kuhusu faida za kunywa dawa ya hydroxychloroquine, Bwana Trump alisema: "Ushahidi wangu ndio huu: Napigiwa simu nyingi sana zinazosifu dawa hii."

Aliongeza: "Nimesikia mengi mazuri kuhusu dawa hii ya hydroxychloroquine na ikiwa siyo nzuri, nawaarifu kwamba sitadhurika."

Ingawa kuna baadhi ya watu waliothibitishwa kupata maambukizi ya virusi vya corona, rais alisema tena Jumatatu kwamba hana dalili zozote na huwa anapimwa kila wakati.
 
Via BBC