Header Ads Widget

SHIRIKA LA SHDEPHA+KUTEKELEZA MRADI WA BADILISHA TABIA EPUKA COVID 19



Mkuu wa wilaya ya Mbogwe mkoa wa Geita , Martha Mkupasi akizungumza baada ya kupokea  mradi wa Badirisha Tabia epuka Covid-19 toka shirika la SHDEPHA+Kahama utakao toa elimu kwa jamii vijijini  kwa miezi mitatu

Na Patrick Mabula , Mbogwe.

Shirika lisilokuwa la Kiserikali la SHDEPHA+  linalotekeleza mradi wa badilisha tabia epuka Covid-19 wilaya ya Mbogwe mkoa wa Geita limetoa wito kwa jamii kuishi kwa kuzingatia maelekezo yaliyotolewa na Serikali na watalaamu wa afya ili  kuepukana na maabukizi ya ugonjwa wa Corona. 

Akitambulisha mradi huo kwa Mkuu wa wilaya ya Mbogwe meneja mradi wa shirika la SHDEPHA+ , Martini Nyakitina amesema mradi huo wa miezi mitatu utakuwa ukitoa elimu kwa jamii inayoishi  mjini na vijijini katika kuunga mkono jitihada za serikali katika kupambana na ugonjwa wa Corona.

Nyakitina amesema katika mradi huo wakati wa kutoa elimu watashirikiana na wahudumu wa afya na vikundi katika kutoa elimu kwenye jamii kuhusu kujikinga na maabukizi ya virusi vya Covid-19 itakayowasaidia siku zote kuishi kwa tahadhali siku zote.

Akipokea mradi huo wenye thamani ya Shilingi milioni 30 , mkuu wa wilaya ya Mbongwe , Martha Mkupasi amesema kwenye jamii bado kunachangamoto katika kujikinga na maabukizi ya virusi vya Covid- 19 vya homa kali ya mapafu Corona hivyo elimu hiyo itawasaidia kujikinga na ugonjwa huo.
Mkuu wa wilaya amelishukuru shirika la SHDEPHA+ kwa mradi huo kwani pia limetoa  msaada wa ndoo za maji pamoja na vitakasa mikono vitakavyopelekwa kwenye mikusanyiko ya watu katika minada na magulio. 

Meneja mradi wa Badirisha Tabia Epuka Covid-19 wa Shirika la SHDEPHA+  Kahama , Martini  Nyakitina wa kwanza kulia akitambulisha mradi wa badilisha tabia epuka Covid 19 kwa mkuu wa wilaya ya Mbogwe mkoani Geita ,Martha Mkupasi

Mkuu wa wilaya ya Mbogwe mkoa wa Geita Martha Mkupasi akipokea msaada wa ndoo za maji pamoja na vitakasa mikono kutoka kwa meneja mradi wa Badilisha tabia epuka  Covid_19  Martini Nyakitina wa shirika la SHDEPHA+ , Kahama utakaotoa elimu kwa wananchi vijijini kuishi kwa tahadhali na kujikinga na ugonjwa wa Corona.