Header Ads Widget

DOCTORS WITH AFRICA/CUAMM YATOA MAFUNZO YA KUKABILIANA NA CORONA SIMIYU


Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dr Festo Dugange
Na Mwandishi wetu Simiyu. 
Wahudumu wa  Afya Ngazi ya Jamii Wapatao 72,  Kutoka  Wilayani Itilima Mkoani Simiyu, wamepewa mafunzo ya kukabilina na Ugonjwa wa Covid 19, unaosababishwa na Virusi Vya Corona, huku wakiombwa  kuwa mstari wa mbele kuisaidia Serikali katika Mapambano ya kudhibiti Ugonjwa huo ambao umekuwa janga la Dunia

.

Akifungua mafunzo hayo yaliandaliwa na Shirika la Doctors With Africa /CUAMM kupitia mradi wa Test and Treat   Mganga Mkuu wa Mkoa huo, Dk Festo Dugange amesema kuwa  wahudumu wa afya ngazi ya Jamii wanaoa wajibu mkubwa wa kuielimisha jamii katika masuala mbalimbali ikiwemo kuchukua tahadhari ya ugonjwa wa Covid 19.
Dr  Dugange amesema ni muhimu wahudumu ngazi ya jamii kusaidiana na Serikali katika mapambano ya kudhibiti Corona, kwani wahudumu hao ndio wanaishi karibu na wananchi Maneneo ya vijijini na mijini hivyo ni vema mafunzo wanayoyapata yakatumika kwa tija na faida kwa jamii inayowazunguka.
“Jamani nyie wahudumu wa afya ngazi  ya jamii ndio mnaishi karibu na wananchi. hapa leo mnapewa mafunzo na Shirika la CUAMM, haya mafunzo ni muhimu kwa jamii mnayoishi nayo, Naomba mkayatumie vizuri kuhakikisha mnaisaidia serikali na Jamii kukabiliana na ugonjwa wa Covid 19,”amesema  Dk. Dugange
Kwa upande wake  Mratibu wa Shughuli  za Kijaamii kupitia Mradi wa Test and Treat kutoka Shirika la Doctors With Africa/ CUAMM,  Gasaya Msira amesema lengo lao ni kushirikiana na Serikali katika mapambano mbalimbali ambapo hufanya shughuli katika  Mkoa miwili ya  Simiyu na Shinyanga ambapo Shinyanga zinafanyika katika Wilaya za  Shinyanga Manispaa,Shinyanga Vijijini na Mkoa wa Simiyu zikifanyika  Wilaya za  Bariadi Mjini na Vijijini .
“Kwa kuwa tunafanya kazi na Serikali tumeona ipo haja kushirikina na Serikali katika mapambano dhidi ya Corona kwa kutoa elimu kwa wadumumu wa afya ngazi ya jamii, hawa wahudumu wataisaidia Serikali   kutoa elimu katika jamii inayowazungunga na jinsi ya kukabilina na ugonjwa huo.”amesema Msira
Msira amesema mpaka sasa wametoa mafunzo kwa wahudumu wa afya ngazi ya jamii  72 katika Wilaya ya Itilima, ambapo hata hivyo watatoa mafunzo baadaye kwa wahudumu 55 wa Wilaya ya Bariadi Mjini, 49 Bariadi Vijijini  huku tayari wakiwa wametoa Mafunzo kama hayo kwa Mkoa wa Shinganya  ambapo Wilaya ya Shinyanga Mjini na Vjijini wahudumu 109 kwa pamoja wamepata mafunzo hayo.
Awali  akizungumza na wahudumu hao wa afya ngazi ya jamii  Mkoa wa Simiyu, Meneja miradi anayeondoka Bi  Veronica Censi amewashukuru wahudumu hao, kwa kufanya kazi pamoja katika kipindi chake  chote alichokuwa  Mtawala  na kwamba anajivunia ushirikiano aliyokuwa akiupata toka kwao.
“Naomba umie fulsa hii kuwashukuru wote, tumefanya kazi kwa pamoja na kwa ushirikiano mkubwa. Najivunia kwa kiasi kikubwa kuwa nanyi hapa Simiyu. Nitawakumbuka na nitaendelea kuwa pamoja nanyi  asanteni sana nawashukuru,”amesema Censi
Shirika la Doctors with Africa/CUAMM limekuwa miongoni mwa Mashirika yasiyo ya Kiserikali yanayoiunga mkono Serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania katika masuala na Nyanja tofauti tofauti ikiwemo sekta ya Afya,Elimu na Maji.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dr Festo Dugange akisisitiza jambo wa Washiriki wa Mafunzo hayo Mjini Bariadi.

Meneja Miradi wa Shirika la Doctors with Africa/CUAMM Bi Veronica Censi anayemaliza muda wake akiwaaga na kuwashukuru washirika hao kwa muda wote aliofanya nao kazi.
Mratibu wa Shughuli  za Kijaamii kupitia Mradi wa Test and Treat kutoka Shirika la Doctors With Africa/ CUAMM,  Gasaya Msira akiwaasa wanajamii hao kwenda kutekeleza elimu waliyoipata kwa vitendo.

Kushoto ni Meneja Miradi wa CUAMM Anayeondoka Bi Veronica Censi na anayefuata ni Mganga mkuu wa mkoa wa Simiyu Dr Festo Dugange. 
 washiriki wa mafunzo ya ngazi ya jamii wakiendelea na Mafunzo
 Mmoja wa Washiriki akifuatilia hatua kwa hataua ya elimu wanayopewa 


 Mtalaam wa Masuala ya Jamii toka CUAMM akiendelea kutoa elimu kwa ukaribu na Mhudumu wa Afya ngazi ya Jamii