
Kutokana na kulipuka kwa maambukizi zaidi kwenye nchi za Amerika Kusini na ya kati, idadi ya watu walioambukizwa virusi vya corona duniani kote sasa inakaribia milioni 5.2 na watu zaidi ya 337,000 wameshakufa. Nchini Brazil pekee idadi ya watu waliokufa imepindukia watu 20,000. Watu wengine 310,000 wameambukizwa nchini humo. Sasa nchi hiyo inashika nafasi ya tatu duniani kwa maambukizi, ikizifuatia Marekani na Urusi.
Mkururugenzi wa kitengo cha hali ya dharura kwenye shirika la afya duniani Mike Ryan amethibitisha kwamba Amerika ya Kusini sasa imekuwa kitovu cha maradhi ya Covid -19. Ameeleza kuwa wameshuhudia kuongezeka kwa maambukizi katika nchi nyingi za Amerika Kusini, hata hivyo amesema Brazil ndiyo iliyoathirika zaidi kwa sasa.
Wakati huo huo nchini Marekani rais Donald Trump anayedhamiria kutafuta njia ya kuondokana na mgogoro wakati ambapo anakabiliwa na changamoto ya kutaka kuchaguliwa tena, ameongeza shinikizo kwa serikali za majimbo na za mitaa ili kulegeza hatua za karantini. Janga la corona limeuathiri uchumi wa Marekani kwa kiwango kikubwa kiasi kwamba miito inatolewa juu ya kulegeza hatua hizo licha ya kuongezeka kwa maambukizi. Watu zaidi ya Milioni 1.6 wameambukizwa virusi vya corona nchini humo na zaidi ya watu 96,000 wameshakufa
Chanzo ni 👇
https://m.dw.com/sw/amerika-ya-kusini-sasa-yaongoza-kwa-maambukizi-ya-corona/a-53546125