` WARAIBU WA DAWA ZA KULEVYA WAMSHUKURU KAMISHNA JENERALI KWA KUDHIBITI WAUZAJI NA WASAMBAZAJI

WANDAMAN HOTEL

WARAIBU WA DAWA ZA KULEVYA WAMSHUKURU KAMISHNA JENERALI KWA KUDHIBITI WAUZAJI NA WASAMBAZAJI

Na Neema Sawaka,Kahama

Waathirika na waraibu  wa dawa za kulevya  wanaopatiwa  matibabu katika kituo cha  Tiba na huduma  kwa waraibu kilichopo katika hospital ya manispaa  ya kahama mkoani Shinyanga wamemshukuru  kamishna Jenerali wamamlaka ya kudhibiti  kupambana na madawa ya kulevya  Aretas James  Lyimo kwa juhudi zinazoendelea za kudhibiti biashara ya usambazaji na uuzwaji wa dawa zakulevya nchini.

Wamesema hatuazinazochukuliwa na  serikali dhidi  ya wauzaji na wasambazaji  wa dawa hizo zimekuwa na mchango mkubwa katika kupunguza na   kukomesha upatikanaji wa madawa ya kulevya ,na kuwapa fursa waathirika kupata matibabu na kurejea katika maisha ya kawaida.

Hayo yamebainika wakati mwenge wa uhuru ulipozindua  jengo la kituo cha  Tiba na huduma  kwa waraibu wa dawa za kulevya  kilichopo  hospital ya manispaa  ya Kahama ,lililojegwa kwa lengo la kutoa huduma za matibabu na

 urekebishwaji wa afya kwa waathirika wa dawa za kulevya.

Jengo hilo ambalo limegharimu  shilingi  milioni 467,fedha zilizotolewa na serikali kupitia mamlaka ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya ,kwa len go la  kuimarisha huduma kwa watu walioathirika na matumizi ya dawa hizo,

Aidha kituo hicho kinasaidia waathirika kupata matibabu  na huduma mbalimbali  zinazolenga kurejesha afya zao ,kwakuwawezesha  kuacha  matumizi ya dawa za kulevya  nahatimaye  kurejea katika shughuri za kawaida za  kijamii na kiuchumi. 

Kwa upande wake Muuguzi kiongozi  wa kituo hicho Grace Nzagamba amesema kituo hicho kwa sasa kinahudumia  kati ya  waraibu 30 _48  ,huku mwitikio wa wananchi  wanaohitaji huduma kuendelea kuwa mkubwa .

Amesema baadhi ya waliowahi kupata matibabu katika kituo hicho  ,wamefanikiwa kuacha  matumizi  ya dawa za kulevya na kurejea katika  maisha ya kawaida huku wengine matibabu  na. ufuatiliaji.

"Baadhi ya waliomaliza matibabu wamepona na sasawanaendelea na shughuli Mbali mbali za kujenga  Taifa alisema Grace Nzagamba

Kwa upande  wake,mmoja wa waathirika hao Multaz Maganga,amesema Alianza kutumia dawa za kulevya mwaka 2005,  lakini kwa sasa  kaacha matumizi hayo 

Amesema hali ya upatikanaji wa dawa za kulevya  kwa sasa si kama ilivyokuwa miaka 3 ya  nyuma na kueleza kuwa hatua za kudhibiti  zimechangia  kupunguza upatikanaji wake.


Multaz amesema  juhudi za serikali  kupitia kamishina lyimo imekuwa mhimu katika kuwasaidia waathirika kupata nafasi ya kuacha matumizi na kuanza maisha  mapya.

 Kwa upande wake Kiongozi wa mbio za Mwenge  wa uhuru kitaifa, Wazo Mwang'onda,amepongeza ujenzi wa kituo hicho na juhudi zilizofanywa katika  kutoa matibabu  kwa waraibu wa dawa za kulevya.

Amesema  ni mhimu  kwa waraibu  wanaopona  na kurejea kwenye hali zao za kawaida  kupewa fursa za kiuchumi ili waweze kujitegemea na  kuendelea kushiriki katika shughuli za  maendeleo ya Taifa.  

Ameeleza kuwa waraibu wanapaswa kuwekewa programu  mbalimbali za kuwawezesha kiuchumi ikiwepo  mikopo  ya asilimia 10 inayotolewa kwa makundi   ya vijana wanawake na watu wenye ulemavu ili waweze kuanzisha shughuri  za uzalishaji.

Aliongeza kuwa uwepo wa kituo hicho   umeonekana  kuwa hatua muhimu  katika kuunganisha juhudi  za kuzuia  dawa za kulevya,kwa kutoa matibabu kwa waathirika na kuwawezesha waliopona kurejea katika maisha yenye tija,huku wana nchi wakihimizwa kuendelea kushirikiana na serikali kwa kutoa taarifa  kuhusu biashara za usambazaji wa dawa hizo.

Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464