` UMOJA NA MSHIKAMANO NI MSINGI WA MAENDELEO YA TAIFA

WANDAMAN HOTEL

UMOJA NA MSHIKAMANO NI MSINGI WA MAENDELEO YA TAIFA


 


Umoja na mshikamano miongoni mwa wananchi ni nguzo muhimu katika kufanikisha maendeleo ya taifa, huku wito ukitolewa kwa kila Mtanzania kuendelea kuilinda na kuitunza amani iliyopo ili kudumisha mazingira bora ya kiuchumi na kijamii.

Akizungumza katika mahojiano maalum, mchimbaji mdogo wa madini Shinyanga David Elias amesema kuwa amani ndiyo inayowawezesha wananchi kufanya shughuli zao kwa uhuru na utulivu, jambo linalochochea uzalishaji na kukuza kipato .

Amesema ni jukumu la kila mwananchi kuhakikisha  analinda amani kwa nguvu zote, akibainisha kuwa bila amani hakuna kazi yoyote inayoweza kufanyika kwa ufanisi, hali ambayo inaweza kurudisha nyuma juhudi za maendeleo.

“Mazingira ya amani yanatupa fursa ya kufanya kazi zetu kwa utulivu kabisa bila usumbufu wowote. Tunapata muda wa kuzalisha na kuboresha maisha yetu na familia zetu,” amesema mchimbaji huyo.

Amesema kukosekana kwa amani kunaweza kusababisha hali mbaya ikiwemo watu kuishi kwa hofu na hata kulazimika kukimbia makazi yao, hali ambayo inaweza kuifanya jamii kugeuka kuwa kama wakimbizi ndani ya nchi yao wenyewe.

Ameongeza kuwa mshikamano wa kijamii unapaswa kuendelezwa kwa kuvumiliana, kuheshimiana na kushirikiana katika shughuli mbalimbali za maendeleo, hatua itakayosaidia kuimarisha umoja wa kitaifa.

Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464