.jpg)
VIJANA wa Manispaa ya Kahama Mkoani Shinyanga wametakiwa Kushiriki Katika kufanya Ibada ili kuishi maisha yatakayo mpendeza Mungu pamoja na Jamii inayowazunguka.
Hayo yamesemwa na mchungaji Constatine Budaga katika Ibada iliyofanika Siku ya jumapili ya kwanza ya Mwaka 2026 katika kanisa la Horeb Internation Church lilipo Kata ya Busoka wilayani ya Kahama,
Budaga amesema kuwa vijana wapaswa kuwa karibu na mungu hasa kwa kufanya ibada itakayo wasaidia kuwajenga kiroho katika maisha yao pamoja na jamii inayowazunguka.
Mchungaji Budaga amesisitiza vijana kuendelea kulinda amani ya nchi na huku akiwataka vijana kukataa kutumika kinyume na makusudio.
Baadhi ya Waamini ambao ni Vijana kutoka katika kanisa hilo Joan John na Zipora Musa wamesema kuwa vijana wanapaswa kuwa mfano mzuri katika jamii na kuacha mambo ambayo yanaweza kuwaingiza katika matatizo na hivyo wanapaswa kuishi katika misingi itakayo mpendeza mungu kwani taifa lolote linategemea vijana waadilifu ili kujenga taifa bora.
mwisho.
Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464