` WALISEMA NIMEROGWA SITAWI KUOLEWA

WALISEMA NIMEROGWA SITAWI KUOLEWA


Jina langu ni Sharon kutoka Nakuru. Kwa muda mrefu nilikuwa natamani sana kuolewa, lakini kila uhusiano niliouanzisha haukudumu. Wanaume walianza kwa upendo mwingi, kisha ghafla wananiacha bila sababu ya kueleweka. Nilijaribu kuomba ushauri kwa marafiki na hata kwa wachungaji, lakini hali iliendelea kuwa ile ile. Kila nilipoona rafiki yangu akiolewa, nilijikuta nalia usiku kucha nikijiuliza ni kwa nini bahati haikunichekea mimi.

Kuna wakati nilifikiria labda tatizo ni mimi, nikabadilisha kila kitu kuhusu maisha yangu. Nilijaribu mavazi tofauti, kujipamba zaidi, hata kujiunga na vikundi vya kina dada ili nijue “mambo ya ndoa.” Lakini bado wanaume walinishirikisha hadi pale mambo yalipokuwa makubwa, kisha wakapotea. Wengine waliniahidi pete, lakini waligeuka dakika za mwisho. Nilihisi nimechoka na nikaamua sitapenda tena, maana moyo wangu ulikuwa umejaa maumivu na mashaka.


Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464