` TANZANIA YATAJWA NCHI YENYE AMANI ZAIDI AFRIKA MASHARIKI

TANZANIA YATAJWA NCHI YENYE AMANI ZAIDI AFRIKA MASHARIKI


Tanzania yatajwa nchi yenye amani zaidi Afrika Mashariki
Tanzania yatajwa nchi yenye amani zaidi Afrika Mashariki

Tanzania imeendelea kung’ara kama taifa linaloongoza kwa amani katika Afrika Mashariki, kwa mujibu wa Ripoti ya Global Peace Index (GPI) ya mwaka 2025, ambapo imeshika nafasi ya 73 kati ya mataifa 163 duniani.

Pamoja na mafanikio hayo kikanda, ripoti hiyo imebainisha kuwa Tanzania imeshuka kwa nafasi nane kimataifa, ikilinganishwa na nafasi ya 65 iliyokuwa nayo mwaka 2024.

Global Peace Index ni ripoti inayotolewa kila mwaka na taasisi ya Institute for Economics and Peace (IEP), ikipima kiwango cha amani kwa kutumia vigezo mbalimbali kama vile usalama wa jamii, migogoro ya ndani na nje, pamoja na kiwango cha kijeshi.

Katika Afrika Mashariki, Tanzania imewashinda majirani zake wote, ikiwemo Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, na Sudan Kusini, ambao wengi wao wameendelea kukabiliwa na changamoto za kiusalama na kisiasa.


SOMA ZAIDI CHANZO NIPASHE

Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464