
FEDHA ZA WAKULIMA 152
KIASI CHA MILION 151 ZAFUNJWA NA VIONGOZI WA AMCOS -USHETU
Na Estomine Henry.
Viongozi wa chama cha
msingi Ibambala Halmashauri ya ushetu, wilayani kahama mkoani Shinyanga wamebainika kugawana fedha za wakulima wapatao
152 sawa na kiasi cha shilingi milioni 151.53 zilizotolewa na kampuni ya Alliance
One kama fidia kwa wakulima wa zao la tumbaku waliopata hasara kutokana na
mafuriko yaliyotoekea katika msimu wa kilimo wa mwaka 2023/2024 na kusababisha hasara.
Hayo yameelezwa leo Mei 27, 2025 na Mkuu wa Taasisi
ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Shinyanga, Donasian Kessy wakati
akiwasilisha taarifa ya robo ya tatu ya kipindi cha januari hadi machi kwa
mwaka 2024/2025 kupitia vyombo vya habari.
“TAKUKURU imebaini kuwa kiasi kikubwa cha fedha,
shilingi milioni 151.53 kiligawiwa kwa watu wasio stahili, wakiwemo ndugu wa
viongozi hao” amesema Kessy
Kessy amesema, TAKUKURU
ilibaini kuwa shilingi milioni 11.62 zilichukuliwa na baadhi ya viongozi wa
chama hicho kwa matumizi yao binafsi, akiwemo Katibu Meneja Bw. Charles Alex
Shiyengo na Mwenyekiti Bi. Faida Paulo Deva
"Miongoni
mwa waliopokea fedha hizo ni Bi. Lucy Masanja Gidabita, mke wa Katibu Meneja,
ambaye alipokea shilingi milioni 34.58, pamoja na Bw. Charles Charles Masanja
aliyelipwa shilingi milioni 5.58.
Kessy
amesema hatua za awali za kurejesha fedha hizo zimeanza kuchukuliwa huku
wahusika wakikabiliwa na hatua za kisheria",ameongeza
Kwa upande mwingine,Takukuru
Shinyanga pia imepokea jumla ya taarifa 57 za tuhuma za rushwa, ambapo 52
zilifanyiwa uchunguzi na 13 kati yake zimefikishwa mahakamani.
Vile
vile, Taasisi hiyo imeweza kutoa wa elimu kwa umma kwa kuendesha imeendesha
mikutano ya hadhara 61, semina 30, na vipindi vya redio na runinga 13 kupitia
programu yao ya Takukuru Rafiki, lengo likiwa ni kuwahamasisha wananchi kushiriki
kikamilifu katika mapambano dhidi ya rushwa.
Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464