Mchome aivimbia CHADEMA kumvua uongozi

Lembrice Mchome, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilaya ya Mwanga, aliyeng'olewa madarakani leo na Baraza la Mashauriano Mkoa wa Kilimanjaro, amesema anatambua kuwa yeye bado ni kiongozi halali wa chama wilayani humo.
Akizungumza na Nipashe Digital amesema: "Sijapokea barua yeyote, sijapokea taarifa yeyote, mimi ninachotambua bado ni kiongozi wa Wilaya ya Mwanga."