`
SHIRIKIANENI NA MFANYE KAZI KWA KARIBU NA OFISI YA CAG - RC MACHA
Home
About
Contact
Home-icon
SHINYANGA
HABARI
MAGAZETI
SIASA
MATUKIO
MICHEZO
MICHEZO
Home
habari
SHIRIKIANENI NA MFANYE KAZI KWA KARIBU NA OFISI YA CAG - RC MACHA
SHIRIKIANENI NA MFANYE KAZI KWA KARIBU NA OFISI YA CAG - RC MACHA
Friday, June 28, 2024
SHIRIKIANENI NA MFANYE KAZI KWA KARIBU NA OFISI YA CAG - RC MACHA
Na. Paul Kasembo, KAHAMA MC.
MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amewataka watalaam wakiongozwa na Wakurugenzi wao kubadilika na kuanza kushirikiana na kufanya kazi kwa karibu zaidi wakati wote na ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) ili waweze kuzipunguza kama siyo kuziondoa hoja zote badala ya kusubiria wakati wa ukaguzi ili waanze kupambana kujibu wakati nafasi ilikuwepo ya kufanya hivyo awali.
RC Macha ameyasema haya leo tarehe 28 Juni, 2024 alipokuwa akifunga mkutano maalum wa baraza la madiwani katika Manispaa ya Kahama ikiwa ni hitimisho la mikutano maalum ya CAG kwa Halmashauri zote sita (6) zinazounda Mkoa wa Shinyanga huku akisisitiza umuhimu wa waheshimiwa madiwani kusimamia miradi ya maendeleo kwa wananchi wao ili waweze kuaminika na kupata hati safi za vipimo vya wananchi na wapate ridhaa tena ya kuongoza ukizingatia kuwa wananchi nao wanayo nafasi ya kupimwa kwa wananchi wao.
"Niwashauri sana wataalam wetu mkiongozwa na wakurugenzi wenu mbadilike na muanze kushirikiana kwa kufanya kazi kwa karibu zaidi wakati wote na ofisi ya CAG ili itakapofika wakati wa ukaguzi muweze kuziondoa kama siyo kuzifuta hoja zote badala ya kusubiria ufike muda wa ukaguzi ndiyo muanze kupambana kuziondoa wakati mlikuwa na hiyo nafasi kufanya kazi pamoja na kushirikiana," amesema RC Macha.
Aidha RC Macha ameitaka Manispaa ya Kahama kuhakikisha wanavipata vikundi vyote vioivyotajwa kuwa havionekani baada ya kukopa fedha kutoka kwenye mfuko wa asilimia 10 ambapo wanawake 4%, vijana 4% na watu wenye ulemavu 2% ili waweze kuzirejesha pamoja na kujibu hoja ya CAG inayotokana na madeni hayo.
Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mapendekezo ya CAG kwa 2022/2023 Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu ndg. Godwin Dinda kwa niaba ya Mkurugenzi ndg. Masudi Kibeto amesema kuwa Manispaa ya Kahama ilikuwa na hoja 25 ambapo hoja 9 zimejibiwa na kufungwa, huku 12 zikiwa kwenye utekelezaji, hoja 3 hazijatekelezwa na hoja 1 imejirudia.
Akiahirisha baraza Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kahama Mhe. Yahaya Bundala amesema kuwa wamepokea pongezi zote kwa kupata hati safi mfululizo, wamepokea maelekezo, ushauri na mapendekezo yote yaliyotolewa na viongozi na kwamba wanakwenda kuyatekeleza kikamilifu ili mwaka wa fedha ujao wasiwe na hoja kabisa.
Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464
TAFUTA HABARI
Wasiliana nasi WhatsApp
AFRICA HEALTH AGENDA
DONATE: CRDB BANK ACCOUNT-01J2058535400, PIGA NAMBA-0788 -469464
HABARI ZILIZOSOMWA SANA
MAHAFALI YA SHULE YA AWALI NA MSINGI KOM MAMBO NI MOTO WAZAZI WAFURAHIA UBORA WA TAALUMA
Saturday, September 20, 2025
SHYDC WAJIVUNIA SHULE YA AWALI NA MSINGI OLA KUFANYA VIZURI KITAALUMA
Saturday, October 04, 2025
KOCHA TIMU YA PAMBA JIJI AIKUBALI TIMU MPYA YA STAND UNITED CHAMA LA WANA
Saturday, October 04, 2025
KISHAPU YAADHIMISHA SIKU YA USAFISHAJI MAZIGIRA DC MASINDI AONYA VIKALI UCHAFUZI WA MAZINGIRA
Saturday, September 20, 2025
SOMA VICHWA VYA MAGAZETI YA LEO SEPTEMBA 20,2025
Friday, September 19, 2025
WASILIANA NASI
Name
Email
*
Message
*
TAGS
habari
4437
magazeti
1245
Kitaifa
483
michezo
314
siasa
113
burudani
89
matukio
77
Afya
46
elimu
22
Makala
20
SIMULIZI
17
biashara
14
mapenzi
10
MICHEZO NA BURUDANI
7
uwekezaji
4
SHINYANGA-UKATILI
3
UKATILI
3
AJIRA
2
HABARI MATUKIO
1
LISHE-UKATILI
1
MAJI
1
MILA NA DESTURI
1
SHINYANGA-WATOTO KIKE
1
SHNYANGA
1
UDUMAVU-WATOTO
1
UKATILI KIJINSIA
1
Unyanyasaji kijinsia vyuoni
1
Ustawi jamii
1
WATOTO
1
WATOTO WENYE ULEMAVU
1
Social Plugin