`
SHIRIKIANENI NA MFANYE KAZI KWA KARIBU NA OFISI YA CAG - RC MACHA
Home
About
Contact
WANDAMAN HOTEL
Home-icon
SHINYANGA
HABARI
MAGAZETI
SIASA
MATUKIO
MAZINGIRA
MICHEZO
Home
habari
SHIRIKIANENI NA MFANYE KAZI KWA KARIBU NA OFISI YA CAG - RC MACHA
SHIRIKIANENI NA MFANYE KAZI KWA KARIBU NA OFISI YA CAG - RC MACHA
Friday, June 28, 2024
SHIRIKIANENI NA MFANYE KAZI KWA KARIBU NA OFISI YA CAG - RC MACHA
Na. Paul Kasembo, KAHAMA MC.
MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amewataka watalaam wakiongozwa na Wakurugenzi wao kubadilika na kuanza kushirikiana na kufanya kazi kwa karibu zaidi wakati wote na ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) ili waweze kuzipunguza kama siyo kuziondoa hoja zote badala ya kusubiria wakati wa ukaguzi ili waanze kupambana kujibu wakati nafasi ilikuwepo ya kufanya hivyo awali.
RC Macha ameyasema haya leo tarehe 28 Juni, 2024 alipokuwa akifunga mkutano maalum wa baraza la madiwani katika Manispaa ya Kahama ikiwa ni hitimisho la mikutano maalum ya CAG kwa Halmashauri zote sita (6) zinazounda Mkoa wa Shinyanga huku akisisitiza umuhimu wa waheshimiwa madiwani kusimamia miradi ya maendeleo kwa wananchi wao ili waweze kuaminika na kupata hati safi za vipimo vya wananchi na wapate ridhaa tena ya kuongoza ukizingatia kuwa wananchi nao wanayo nafasi ya kupimwa kwa wananchi wao.
"Niwashauri sana wataalam wetu mkiongozwa na wakurugenzi wenu mbadilike na muanze kushirikiana kwa kufanya kazi kwa karibu zaidi wakati wote na ofisi ya CAG ili itakapofika wakati wa ukaguzi muweze kuziondoa kama siyo kuzifuta hoja zote badala ya kusubiria ufike muda wa ukaguzi ndiyo muanze kupambana kuziondoa wakati mlikuwa na hiyo nafasi kufanya kazi pamoja na kushirikiana," amesema RC Macha.
Aidha RC Macha ameitaka Manispaa ya Kahama kuhakikisha wanavipata vikundi vyote vioivyotajwa kuwa havionekani baada ya kukopa fedha kutoka kwenye mfuko wa asilimia 10 ambapo wanawake 4%, vijana 4% na watu wenye ulemavu 2% ili waweze kuzirejesha pamoja na kujibu hoja ya CAG inayotokana na madeni hayo.
Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mapendekezo ya CAG kwa 2022/2023 Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uhasibu ndg. Godwin Dinda kwa niaba ya Mkurugenzi ndg. Masudi Kibeto amesema kuwa Manispaa ya Kahama ilikuwa na hoja 25 ambapo hoja 9 zimejibiwa na kufungwa, huku 12 zikiwa kwenye utekelezaji, hoja 3 hazijatekelezwa na hoja 1 imejirudia.
Akiahirisha baraza Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kahama Mhe. Yahaya Bundala amesema kuwa wamepokea pongezi zote kwa kupata hati safi mfululizo, wamepokea maelekezo, ushauri na mapendekezo yote yaliyotolewa na viongozi na kwamba wanakwenda kuyatekeleza kikamilifu ili mwaka wa fedha ujao wasiwe na hoja kabisa.
Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464
MRADI WA MTOTO KWANZA
TAFUTA HABARI
Wasiliana nasi WhatsApp
ELIMU YA MALEZI NA MAKUZI KWA UMMAA KUPITIA VYOMBO VA HABARI
DONATE: CRDB BANK ACCOUNT-01J2058535400, PIGA NAMBA-0788 -469464
HABARI ZILIZOSOMWA SANA
WACHIMBAJI WADOGO NZEGA WARUDISHA FAIDA KWA JAMII WAKABIDHI MADAWATI 289 SERIKALINI,WAPANDA MITI KUTUNZA MAZINGIRA
Saturday, May 30, 2026
WAZIRI WA FEDHA KUONGOZA UJUMBE WA TANZANIA MIKUTANO YA IMF NA BENKI YA DUNIA
Monday, April 13, 2026
Tanzia : RPC TABORA SACP RICHARD ABWAO AFARIKI DUNIA
Saturday, June 20, 2026
SOMA VICHWA VYA HABARI MAGAZETI YA LEO MEI 31,2026
Saturday, May 30, 2026
DC MPWAPWA AWATAKA VIJANA KULINDA AMANI NA KUCHANGAMKIA FURSA
Friday, May 29, 2026
WASILIANA NASI
Name
Email
*
Message
*
TAGS
habari
6140
magazeti
1466
Kitaifa
483
michezo
321
siasa
114
burudani
94
matukio
77
Afya
47
elimu
22
Makala
20
SIMULIZI
17
biashara
14
mapenzi
10
MICHEZO NA BURUDANI
8
uwekezaji
4
SHINYANGA-UKATILI
3
UKATILI
3
AJIRA
2
HABARI MATUKIO
2
LISHE-UKATILI
1
MAJI
1
MILA NA DESTURI
1
SHINYANGA-WATOTO KIKE
1
SHNYANGA
1
UDUMAVU-WATOTO
1
UKATILI KIJINSIA
1
Unyanyasaji kijinsia vyuoni
1
Ustawi jamii
1
WATOTO
1
WATOTO WENYE ULEMAVU
1
Social Plugin