Header Ads Widget

RAIS MWINYI AFARIKI DUNIA


 RAIS WA AWAMU YA PILI ALI HASSAN MWINYI AFARIKI DUNIA

Rais Mstaafu wa awamu ya pili wa Tanzania, Ally Hassan Mwinyi amefariki Dunia leo Februry 29,2024 saa 11:30 Jioni katika Hospitali Jijini Dar es salaam alipokuwa akipatiwa matibabu kwa ya ugonjwa wa Saratani ya Mapafu.

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ametangaza msiba huo leo ambapo amesema Mzee Mwinyi alikuwa akipatiwa matibabu tangu November 2023 London Uingereza na baadaye kurejea Nchini na kuendelea na matibabu Mzena Hospital.

Rais Samia ametangaza siku saba za maombolezo kuanzia kesho kufuatia kifo hicho.

Ali Hassan Mwinyi aliyeongoza Serekali ya Awamu ya Pili aliingia madarakani rasmi tarehe 5 Novemba 1985. Alizaliwa tarehe 5 mei, 1925

Post a Comment

0 Comments