Header Ads Widget

MKUTANO MKUU WA TANCOPS WAMUONDOA KWENYE UJUMBE MWENYEKITI WA SIMCU KWA KUKIUKA MAKUBALIANO.

 


Mwenyekiti wa Mkutano Mkuu wa TANCOPS ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika Mbogwe Mkoa wa Geita Elias Madata akizungumza kwenye mkutano huo.

                                        Na Shinyanga Press Club Blog

Mkutano mkuu wa umoja wa vyama vikuu vya ushirika vya Pamba Tanzania (TANCOPS) umemsimamisha na kumuondoa kwenye nafasi ya ujumbe kwenye Ushirika huo Mwenyekiti wa chama kikuu cha ushirika cha mkoa wa Simiyu (SIMCU) Lazaro Walwa kwa madai ya kusaliti ushirika.

 

Hatua hiyo imejadiliwa na wajumbe wa Mkutano huo na kufikia uamuzi wa kumsimamisha baada ya kukiuka makubaliano ya kuuza pamba kilo moja  kwa Sh 1060 na siyo 1057.

 Mwenyekiti wa Mkutano huo  ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika Mbogwe Mkoa wa Geita Elias Madata,amesema  wajumbe wamejadili suala la nidhamu na bei ya pamba na kukubaliana kuandamana hadi ofisi ya Waziri wa Kilimo kumtaka atoe ufafanuzi juu ya baadhi ya tozo zenye ukakasi kwenye ununuzi wa zao la pamba. 

 Katika kikao hicho wajumbe wameukataa mfumo wa ununuzi wa zao la pamba unaojulikana kama Simiyu modo pamoja na kulalamikia tozo zenye ukakasi wakati wa ununuzi wa zao la pamba. 

Naye Mwenyekiti wa Umoja wa vyama Vikuu vya Ushirika wa Pamba Tanzania  Zainab Mahenge,amesema hatua hiyo inalenga kuwasaidia wakulima wasipunjwe kwa kusainishwa mikataba ya Sh 1057 kinyume na makubaliano .

 


Mwenyekiti wa Umoja wa Vyama Vikuu vya Ushirika wa Pamba Tanzania  Zainab Mahenge akizungumzia suala la kuchukuwa hatua ili kuwasaidia wakulima kuuza kwa bei waliyokubaliana.

Mjumbe wa Bodi ya TANCOPS Yahaya Ramadhani akichangia hoja kwenye mkutano

   Baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa umoja wa vyama vikuu vya ushirika vya Pamba Tanzania 






Post a Comment

0 Comments