Header Ads Widget

UVUVI WA DAGAA WASITISHWA MWANZA



Shughuli za uvuvi wa dagaa katika mialo ya Mkoa wa Mwanza zimesitishwa kwa siku 15 kuanzia Januari 24, mwaka huu kutoa fursa samaki hasa dagaa kuzaliana katika kipindi cha mbalamwezi.


Uamuzi huo ni kwa mujibu wa sheria na kanuni za uvuvi na marekebisho yake ya 2020 na kwa mujibu wa Kaimu Ofisa Mfawidhi Ulinzi na Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi Kanda ya Ziwa, Laurent Mbujiro zuio la aina hiyo litafanyika kila mwezi wakati wa mbalamwezi.


“Tunatarajia kufungulia shughuli za uvuvi kuanzia Jumanne (Februari 8). Tunawashukuru wavuvi wa dagaa kwa ushirikiano waliouonyesha kwa kusitisha shughuli kwa siku 15 kuruhusu mazao ya samaki kuongezeka,” alisema Mbujiro.

Soma hapa zaidi chanzo Mwananchi.

Post a Comment

0 Comments