Header Ads Widget

TRA KAHAMA YAWAONYA WAFANYABIASHARA WANAVYODANGANYANA KUHUSU RISITI



 

MKAGUZI MSAIDIZI   WA HESABU KUTOKA  TRA  MKOA WA KIKODI KAHAMA  HONEST MUSHI . 

Na Kareny  Masasy,

MSAIDIZI mkaguzi wa hesabu  kutoka mamlaka   ya  Mapato  Tanzania  (TRA) mkoa wa kikodi  Kahama  Honest Mushi  amesema kuwa  wafanyabishara  wanaamini kuwa wasipo toa risiti   malipo ya kodi yanakuwa kidogo.

Mushi akimwakilisha  meneja  wa mamlaka hiyo  Warioba Kanile katika semina ya wafanyabishara iliyofanyika  leo  tarehe 22/08/2022   ambayo ililenga  kutoa elimu ya mabadiliko ya sheria ya  ulipaji kodi kwa mwaka wa fedha wa 2022 ulioanza mwezi Julai.

“Wafanyabishara wamekuwa wakipotoshana  kuwa  usipotoa risiti  kodi  inakuja ndogo  kitu ambacho siyo kweli  kinachotakiwa waweke rekodi za bidhaa zao vizuri wanazouza  na wahasibu watimize wajibu wao   kitu cha kwanza kwa mfanyabiashara ni kulipa kodi”amesme Mushi .

  Mushi  amesema kuwa wahasibu    wamekuwa wakiongea nao nakukosa majibu  kuhusu upigaji wa hesabu  unaoleta  utata  ndiyo maana mamlaka ya mapato huwa inawataka siku ya  upigaji wa hesabu awepo mpiga hesabu na mfanyabishara mwenyewe.

Mushi amesema kuwa  wapo wahasibu  wazuri waliopata usajili kutoka  mamlaka ya mapato   na leseni   zao kila mwaka zinakwisha muda wake na  kusajiliwa upya  na  mfanyabiashara  anatakiwa kumuandali nyaraka zote  muhimu ili azifanyie kazi  asipompatiwa  ndiyo hapo changamoto inapotokea.

Baadhi ya wafanyabiashara  akiwemo Frank Jerome   ameomba kukombolewa kwa kupatiwa wahasibu  wanaokwenda kukagua hesabu za biashara zao ili kuendana na uhalisia wa biashara.

“ Baadhi ya wahasibu wanakuja kuwafanyia hesabu  sio waaminifu  na matokeo yake mfanyabiashara kwenye  ulipaji   anaelezwa   kulipa   kodi  ya  sh  Millioni 700 sio uongo bali yupo aliyeambiwa kiasi hicho”amesema Jerome .

Mfanyabishara  Arbogast Lyimo  amesema kuwa   wao sio wataalamu wa mahesabu kunapotokea dosari aulizwe mtaalamu aliyepiga hesabu sababu  wanakuwa wamemlipa  pesa  na  wao kutojua chochote.

 


Post a Comment

0 Comments