Header Ads Widget

RUTO ATANGAZWA RAIS MTEULE WA KENYA

Tume ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) ya Kenya, Wafula Chebukati imemtangaza mgombea wa Kenya Kwanza, William Ruto kuwa Rais mteule wa Kenya.
 
Ruto ambaye ni Naibu Rais wa Kenya, ameshinda uchaguzi huo uliokuwa na mchuano mkali kati yake na mgombea wa Azimio la Umoja, Raila Odinga aliyekuwa akipigiwa debe na Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta.


Leo Jumatatu Agosti 15, katika ukumbi wa Bomas uliokuwa ukitumika kwa ajili ya kuhakiki kura za urais, Mwenyekiti wa IEBC, Wafula Chebukati ametangaza matokeo hayo baada ya siku sita za kihoro cha kuyasubiri tangu siku iliyopigwa kura.
 
SOMA ZAIDI HAPA CHANZO MWANANCHI.

Post a Comment

0 Comments