Header Ads Widget

TANZANIA YAFUZU KOMBE LA DUNIA

Timu ya Taifa ya Tanzania ya Wanawake U-17 (Serengeti Girls) imefanikiwa kufuzu Kombe la Dunia baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Cameroon mchezo uliochezwa jioni ya leo kwenye uwanja wa Amaan.

Bao pekee la Serengeti Girls limefungwa na Neema Paul dakika 47 na kuifanya Tanzania itinge Kombe la Dunia litakalochezwa Oktoba mwaka huu nchini India kwa jumla ya mabao 5-1 kufuatia mchezo wa awali kushinda 4-1 ugenini.

Serengeti Girls leo saa 3 usiku watatua kwenye uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar es salaam, wakitokea hapa Zanzibar baada ya kufuzu Kombe la Dunia.


Tanzania ileeee World Cup ya Wanawake U-17.

Hongereni Serengeti Girls kuzidi kuitangaza Tanzania Kimataifa .

Imeandaliwa na Aabubakarkisandu Zanzibar.

Post a Comment

0 Comments