Header Ads Widget

SERIKALI YAJIBU HOJA 5 LOLIONDO, NGORONGORO

SERIKALI YAJIBU HOJA 5 LOLIONDO, NGORONGORO


Serikali ilitumia zaidi ya saa tatu kujibu hoja takriban tano zilizoibuliwa na wanaharakati nchini kuhusu sakata la Loliondo na Ngorongoro huku ikiwaomba mabalozi na wawakilishi wa mashirika mbalimbali ya kimataifa kuamini taarifa inazozitoa.

Serikali imekutana na mabalozi hao baada ya makundi ya wanaharakati na wanasiasa kulalamika juu ya uamuzi wake wa kumega kilometa za mraba 1,500 za ardhi kwa ajili ya kutunza eneo la pori tengefu Loliondo katika Wilaya ya Ngorongoro.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na mabalozi hao jana Dar es Salaam, alisema Serikali inayo dhamira njema katika mpango huo na inazingatia haki za binadamu katika hatua za kuwahamisha, tofauti na taarifa zinazoelezwa na kundi linalopinga mchakato huo.

Kufuatia hatua ya Serikali kuweka amipaka ya eneo hilo, kumeibuka madai ya vurugu wakati wananchi wanapinga hatua hiyo hali iliyosaabisha askari mmoja kuuawa na watu kudhaa kujeruhiwa.
 
SOMA ZAIDI HAPA CHANZO MWANANCHI.

Post a Comment

0 Comments