Header Ads Widget

MWANAFUNZI DARASA LA SABA AUAWA, ANYOFOLEWA MACHO

Mwanafunzi darasa la saba auawa, adaiwa kunyofolewa macho

Mtoto Johnson Thomas (14) mwanafunzi wa darasa la saba katika Shule ya Msingi Buhalahala mjini Geita amekutwa amefariki dunia na mwili wake kutupwa pembeni ya mto karibu na Barabara ya Buhalahala kwenda Kijiji cha Nyakato.


Tukio la mtoto huyo kuuawa ni tukio la tatu ndani ya wiki mbili ambapo watoto wengine wawili mmoja akiwa na miaka miwili aliuawa kwa kukatwa shingo na mwingine wa miaka saba inadaiwa alilawitiwa na kubakwa kisha kukatwa shingo wilayani Nyang’hwale mkoani humo.

Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Henry Mwaibambe amesema tukio hilo limetokea Juni 18 saa 11 jioni katika Kijiji cha Buhalahala.

Amesema mtoto huyo alitoka nyumbani kwao Juni 12 kwa usafiri wa bajajaji akielekea Buhalahala kushona sare za shule na mara ya mwisho alionekana na mwanafunzi mwenzake akielekea barabara inayokwenda ofisi za GPH. Tangu siku hiyo hakurejea mpaka mwili wake ulipopatikana Juni 18.

SOMA ZAIDI HAPA; CHANZO MWANANCHI.

Post a Comment

0 Comments