Header Ads Widget

KONGAMANO LA AIESEC LAFANYIKA CHUO KIKUU CHA DODOMA

Kongamano la kuwajengea uwezo Wanafunzi wa vyuo vikuu kuchangamkia fursa mbalimbali lililoandaliwa na taasisi ya AIESEC Tanzania na kudhaminiwa na kampuni ya Madini ya Barrick, kwa kushirikiana na wadau mbalimbali limefanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).

Katika kongamano hilo wanafunzi walipata nafasi ya kusikiliza mada mbalimbali zilizotolewa na wasomi kutoka kwenye makampuni yanayofanya vizuri ambazo zilijikita kuwajengea uwezo wa kujiamini, kuwa wabunifu sambamba na kusoma kwa bidii ili wasiachwe nyuma katika ulimwengu wa sayansi na teknolojia ili waweze kunufaika na fursa mbalimbali zinazojitokeza pia kuweza kuajirika na kuweza kujiajiri.
Meneja Raslimali Watu wa Mgodi wa Bulyanhulu,Lumbu Kambula akiongea katika kongamano hilo.
Mwanafunzi wa UDOM akiuliza swali wakati wa kongamano hilo.
Baadhi ya Wanafunzi wa UDOM wakifuatilia mada wakati wa kongamano hilo.
Wanafunzi wakiwa katika picha na Afisa wa kampuni ya Barrick.
Baadhi ya Wanafunzi wa UDOM wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa IESEC,Barrick na waliotoa mada mbalimbali katika kongamano hilo.

Post a Comment

0 Comments