Header Ads Widget

RIPOTI YA CAG WAFANYAKAZI TANESCO WALIVYOLIPANA POSHO ZA MABILIONI


TANESCO walivyolipana posho za mabilioni bila kodi

MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) amebaini Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kulipa posho za Sh. bilioni 61.64 kwa wafanyakazi wake pasi na kutoza kodi.



Katika ripoti yake ya ukaguzi kwa mwaka 2020/21 iliyowasilishwa bungeni Jumanne, CAG Charles Kichere anasema amebaini shirika hilo kutotoza kodi ya Sh. bilioni 17.4 kwenye posho za watumishi.

Anafafanua kuwa Kifungu cha 7(1) cha Sheria ya Kodi ya Mapato Sura ya 332 (kama ilivyorekebishwa mwaka 2019) kinasema mapato ya mtu binafsi kutokana na ajira kwa mwaka wa mapato yatakuwa faida aipatayo mtu huyo kutokana na ajira ya mtu huyo kwa mwaka wa mapato.

Vilevile, CAG anasema Kifungu cha 7(3)(k) cha sheria hiyo kinaeleza kuwa katika kukokotoa faida aipatayo mtu binafsi kutokana na ajira, posho ambazo hazijumuishwi (posho zisizo za kodi) ni posho ya nyumba, posho ya usafiri, posho ya uwajibikaji, posho ya kazi ya ziada, posho ya muda wa ziada, posho ya mazingira magumu na honoraria kwa mtumishi wa serikali au taasisi ambazo zinalipwa kutokana na bajeti ya vyanzo vingine vya mapato, yaani bajeti isiyotokana na ruzuku kutoka serikalini.

SOMA ZAIDI HAPA CHANZO NIPASHE.

Post a Comment

0 Comments