Header Ads Widget

ASKOFU KKKT ANG'OLEWA

Mkutano mkuu maalumu wa Dayosisi ya Konde ulioitishwa na Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Fredrick Shoo umemvua wadhifa wa uaskofu, Askofu wa dayosisi hiyo, Edward Mwaikali na kuibua maswali.
 
Wajumbe wa mkutano huo ambao walikuwa ni wale waliohudhuria mkutano mkuu wa dayosisi hiyo mwaka 2017, pia walimchagua kwa kura 2,014, Mchungaji Geofrey Mwakihaba kuwa Askofu mteule wa dayosisi hiyo ya Konde.

Mbali na kumuondoa madarakani Askofu Mwaikali, tume iliyoundwa na mkuu wa kanisa chini ya uenyekiti wa Askofu Alex Malasusa, imerejesha makao makuu ya dayosisi hiyo Tukuyu kutoka Ruanda jijini Mbeya huku utaratibu wa kurudisha kiti cha askofu ukiandaliwa.
 
 SOMA HAPA ZAIDI CHANZO MWANANCHI.
 

Post a Comment

0 Comments