Header Ads Widget

SOMA SAKATA ZIMA LA MGOGORO HIFADHI YA NGORONGORO

Joto la mgogoro wa eneo la Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), limezidi kupanda kutokana na kuongezeka kwa shinikizo la kuitaka Serikali iwaondoe wafugaji wa kijamii ya kimasai ambao idadi yao imekuwa ikizidi kuongezeka siku hadi siku na kutishia uhifadhi wa wanyama katika eneo hilo.

Tayari kuna msuguano mkubwa juu ya hatima ya eneo hilo kutokana na madai kuwa baadhi ya watu wenye idadi kubwa ya mifugo wamewaajiri wafugaji wa kimasai watunze mifugo hiyo katika eneo hilo na hivyo kutishia uhai wa wanyama na mazingira.

Inadaiwa wamiliki hao wa mifugo wamekuwa wakitumia fedha zao kuendesha harakati za kuzuia watu kuondolewa kwenye eneo hilo wakihofia endapo hatua hiyo itatekelezwa watapoteza mifugo yao au mifugo hiyo itakosa malisho ya uhakika wanayoyapata hivi sasa.

Post a Comment

0 Comments