Header Ads Widget

HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA IMETOA MIKOPO YA SHS.MILIONI 173.8 KWA VIKUNDI 16 VYA WANAWAKE NA VIJANA KWA KIPINDI CHA ROBO YA PILI OKTOBA-DESEMBA, 2021/2022


 Picha ya pamoja ya wanufaika wa mikopo,viongozi wa benki ya CRDB na viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga katika zoezi la kupokea hundi ya mikopo iliyotolewa na Halmashauri kupitia benki ya CRDB tawi la Shinyanga.

Upande wa kulia ni Meneja biashara kanda ya Magharibi   kutoka Benki ya CRDB  Jumanne Wagana  akiongea baada ya kukabidhi hundi kwa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga na upande wa katikati ni meneja wa Benki hiyo  tawi la Shinyanga Luther Mneney akiwa na diwani wa kata ya Solwa Awadhi Mbaraka.

Na Mwandishi wetu,

Vikundi 16 vya vijana ,wanawake na  watu wenye ulemavu kutoka Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga vimeweza kunufaika na mikopo wenye thamani ya Shs 173.8  iliyotolewa kipindi cha robo ya pili oktoba-desemba 2021/2022 na Halmashauri  hiyo kwa kupitia  mapato ya ndani.

Hayo yameelezwa Alhamisi 3 ,februari,2022  na Mkurugenzi wa Halmashauri  hiyo Nice Munissy alipokuwa akipokea hundi ya fedha za mikopo iliyokwisha tolewa kwa vikundi vya vijana,wanawake na watu wenye ulemavu na kutoka   Halmashauri hiyo kupitia benki ya CRDB  tawi la Shinyanga iliyokuwa ikitoa huduma za fedha kwa vikundi hivyo.

Hundi hiyo  ilikabidhiwa   na    kwa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo  Nice Munissy  mbele ya  vikundi vya wanawake na vijana  vilivyonufaika na mikopo  kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao za ujasiriamali .

Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Nice Munissy   amesema kuwa  tayari wametoa kiasi cha sh millioni 173.8 ambazo zimetokana na mapato ya ndani  kwa kuwakopesha   wanawake vijana na  watu wenye walemavu kupitia  asilimia kumi ya makusanyo ya Halmashauri hiyo.

“Haijawahi kutokea  kutoa kiasi hicho kwenye makundi maalum ambapo lengo lilikuwa ni kutoa kiasi cha  sh million 192  ambazo wangekopeshwa bila riba  na kundi la walemavu  hawajajitokeza hivi sasa katika kukopa lakini vipindi vingine vya robo mwaka walijitokeza na kukopa sasa wana mradi wa mashine ya kusaga”.

Munissy amesema  kuwa robo ya kwanza ya mwaka 2021/2020 katika makusanyo walishika nafasi ya nane na robo pili wameshika nafasi ya tatu hivyo aliwataka  wanaokopeshwa wajitahidi kurudisha marejesho  na ili kutoa fursa kwa wengine kukopeshwa.

Naye Makamu Mwenyekiti wa  Halmashauri hiyo Isack  Sengerema  amesema kuwa  takwimu  ya juzi  iliyotolewa kuhusu ukusanyaji wa mapato halmashauri imekuwa ya tatu na mwaka uliopita ilikuwa ya mwisho  na ndiyo maana wameona kutoa  fedha kwenye makundi hayo sababu ni kodi zao na wanatakiwa kuzirejesha ili ziweze kuwanufaisha na wengine na fedha hizi walikuwa wapewa wajanja wajanja sasa zinawafikia hata watu wa pembezoni.

Kwa upande mwingine , Said Salehe Mwenyekiti wa Vijana  amesema kuwa  wanaishukuru serikali kwa kuwapatia mikopo ambao haina riba na wamekopa sh million 12 na kununua pikipiki tano ambazo watakuwa wanarudisha marejesho.

Pia Hawa Migeto amesema kuwa kikundi chao  wamekopa kiasi cha sh millioni 15 kwa ajili ya shughuli za ujasirimia mali na watazingatia kuzirejesha ili kuwapa nafasi watu wengine.

Meneja wa tawi la CRDB Mkoa wa  Shinyanga  Bw. Luther Mneney Mneney amesema kuwa  suala la hela linahitaji uaminifu ninyi vikundi ambao mmekopeshwa na mkazifanyie kazi zenye kuwaletea manufaa na kurejesha kwa wakati.

Jumanne  Wagana  Meneja biashara  kanda ya Magharibi  kutoka benki ya CRDB   amepongeza ukusanyaji  wa mapato hayo  na kueleza kuwa   shughuli wanazo ni nyingi na vikundi vingi vimekuwa vikikopa  hasa wale wenye  kipato cha  chini  hivyo amewaomba vikundi hivyo wawe mabalozi kwa wengine  na kufafanua namna ya benki hiyo inavyoweza kutoa  mafao  yenye faida  ikiwemo bima.

Wanavikundi kutoka maeneo tofauti  wakisikiliza kwa makini maelezo wanayopewa dhidi ya mikopo hiyo walikwishapewa.

Makamu Mwenyekiti wa  Halmashauri hiyo Isack Sengerema akiongea kwenye kikao cha kukabidhiwa hundi  huku akiwasisitiza wanavikundi kurejesha kwa wakati.


 



Post a Comment

0 Comments