Header Ads Widget

MADAKTARI WAFUNGUKA KUVUJA MTIHANI WA UTABIBU


Wadau wa sekta ya afya nchini wamestushwa na taarifa za kuvuja kwa mitihani ya wanafunzi wa programu ya utabibu, huku madaktari wakisema ni janga kwa Taifa kwa kuwa walengwa wanahusika na afya za watu.

Moja ya majukumu ya maofisa tabibu ambao wengi wako vituo vya afya na zahanati ni kuona, kumchunguza na kutibu wagonjwa na kufanya upasuaji mdogo, na pale inatotokea suala ni zito kwake, hutoa rufaa ngazi ya juu.

Mtaalamu bingwa wa afya ya jamii nchini, Dk Fidelis Owenya alikwenda mbali zaidi na kusema kama wizara isingebaini mapema na wakahitimu na kuingia kwenye soko, matokeo yake ndiyo yale ya kuwa na tabibu kumwandikia mgonjwa dawa A badala ya dawa B.
 
SOMA ZAIDI HAPA CHANZO MWANANCHI

Post a Comment

0 Comments