Header Ads Widget

DED SHINYANGA NICE MUNISSY AKABIDHI CHAKULA KWA WAHANGA WA MIMBA NA NDOA ZA UTOTONI SHULE YA AGAPE


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe. Nice Munissy (wa pili kushoto) akikabidhi sehemu ya vyakula vyenye thamani ya shilingi Milioni 1.6 kwa ajili ya mabinti waathirika wa ndoa na mimba za utotoni wanaosoma katika shule ya Sekondari ya Agape Knowledge Open School.

Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe. Nice Munissy amekabidhi vyakula vyenye thamani ya shilingi Milioni 1.6 kwa ajili ya mabinti waathirika wa ndoa na mimba za utotoni wanaosoma katika shule ya Sekondari ya Agape Knowledge Open School ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike duniani.

Akizungumza leo Jumamosi Oktoba 16, 2021 wakati wa kukabidhi vyakula hivyo katika shule ya Agape Knowledge Open School iliyopo katika mtaa wa Busambilo kata ya Chibe manispaa ya Shinyanga, Munissy amelishukuru shirika lisilo la kiserikali la Agape AIDS Control Programme (AACP) kwa kuendelea kuwasaidia na kulea mabinti hao waliopata changamoto za ukatili wa kijinsia.

“Sisi Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ni wadau wa haki za mtoto wa kike na baadhi ya mabinti waliopo kwenye shule ya Agape wanatoka Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, hivyo katika kusherehekea Siku ya Mtoto wa kike duniani ambayo hufanyika Oktoba 11 tumeamua kuja hapa ili kuwapatia chakula”,amesema Munissy.

“Tumeleta mchele kilo 500, maharage kilo 500, lita 40 za mafuta ya kupikia na chumvi vyote vikiwa na thamani ya shilingi Milioni 1,690,000/= ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya mtoto wa kike mwaka huu 2021”,ameongeza Munissy.

Aidha amesema serikali itaendelea kutoa ushirikiano kwa shirika la Agape na mashirika mengine ambayo yamekuwa mstari wa mbele katika kumlinda mtoto wa kike na kupinga matukio ya ukatili wa kijinsia.

Mkurugenzi huyo wa Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga amewataka mabinti hao kusoma kwa bidii na kutokubali kurudi nyuma ili waweze kutimiza ndoto zao huku akiwaomba kuwa mabalozi wazuri katika jamii kueleza madhara ya matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

“Sitegemei kuona wala kusikia binti aliyepo katika shule hii anapata mimba au kukatisha masomo na kuolewa, someni kwa bidii huku mkijishughulisha na ujasiriamali,fanyeni kazi za ubunifu ambazo zitawaingizia kipato”,amesema Munissy.

Katika hatua nyingine ameitaka jamii kuachana na vitendo vya kuozesha watoto wadogo kwani kufanya hivyo ni ukatili hivyo wawapeleke shule na kuwapatia mahitaji muhimu ili waweze kutimiza ndoto zao na kwa wale wanaoendekeza vitendo vya ukatili wa kijinsia watachukuliwa hatua za kisheria.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Agape AIDS Control Programme (AACP),linalomiliki shule hiyo,John Myola ameishukuru Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kwa msaada huo wa chakula kwa ajili ya wanafunzi wa kike.

“Tunawashukuru sana Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga kwa kutupatia chakula kwa ajili ya watoto wetu hawa ambao ni waathirika wa matukio ya ukatili wa kijinsia, tunawashukuru sana kwani mmekuwa wadau wazuri, mmekuwa mkitusaidia mara kwa mara hiyo ni kuonesha kwa vitendo kuwa hawa watoto ni wetu sote”,amesema Myola.

Myola amesema hivi sasa katika shule ya Sekondari ya Agape Knowledge Open School iliyoanzishwa mwaka 2014 , sasa wana jumla ya wanafunzi 48 na tangu mwaka 2017 ufaulu wa wanafunzi wa kidato umekuwa mzuri wana uwezo mkubwa darasani ambapo baadhi yao wamejiunga na masomo ya kidato cha tano na wengine vyuo mbalimbali.

Amesela Uwepo wa watoto yatima na waathirika wa ndoa na mimba za utotoni ndiyo ulisababisha shirika la Agape kuanzisha kituo cha elimu ya sekondari cha Agape Knowledge Open School.

Hata hivyo Myola amesema bado shule hiyo inakabiliwa na changamoto ya miundo mbinu ya madarasa hivyo kuwaomba wadau kujitokeza kusaidia shule hiyo ili wanafunzi wawe katika mazingira rafiki zaidi.

Kwa upande wao wanafunzi hao wameishukuru Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kwa kuwapatia chakula huku wakieleza kuwa elimu wanayoipata imewajengea uwezo mzuri wa kujitambua,kufikiri,kufanya maamuzi sahihi na mambo kadha wa kadha ikiwemo elimu ya ujasiriamali,stadi za maisha na stadi za kazi na afya ya uzazi.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe. Nice Munissy akizungumza leo Jumamosi Oktoba 16,2021 wakati akikabidhi vyakula vyenye thamani ya shilingi Milioni 1.6 kwa ajili ya mabinti waathirika wa ndoa na mimba za utotoni wanaosoma katika shule ya Sekondari ya Agape Knowledge Open School ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike duniani. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe. Nice Munissy akizungumza wakati akikabidhi vyakula vyenye thamani ya shilingi Milioni 1.6 kwa ajili ya mabinti waathirika wa ndoa na mimba za utotoni wanaosoma katika shule ya Sekondari ya Agape Knowledge Open School. Kushoto ni Mkurugenzi wa Shirika la Agape, John Myola, kulia ni Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Deus Muhoja.
Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Agape AIDS Control Programme (AACP), linalomiliki ya Sekondari ya Agape Knowledge Open School ,John Myola akizungumza wakati Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe. Nice Munissy (katikati)  akikabidhi vyakula vyenye thamani ya shilingi Milioni 1.6 kwa ajili ya mabinti waathirika wa ndoa na mimba za utotoni wanaosoma katika shule 
 Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Deus Muhoja akizungumza wakati Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe. Nice Munissy (katikati) akikabidhi vyakula vyenye thamani ya shilingi Milioni 1.6 kwa ajili ya mabinti waathirika wa ndoa na mimba za utotoni wanaosoma katika shule ya Sekondari ya Agape Knowledge Open School.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe. Nice Munissy (wa pili kushoto) akikabidhi sehemu ya vyakula vyenye thamani ya shilingi Milioni 1.6 kwa ajili ya mabinti waathirika wa ndoa na mimba za utotoni wanaosoma katika shule ya Sekondari ya Agape Knowledge Open School. Wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Deus Muhoja. Wa kwanza kulia ni Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Bi. Aisha Omary akifuatiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Agape, John Myola na mmoja wa wanafunzi 48 wanaosoma katika shule ya Sekondari ya Agape Knowledge Open School
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe. Nice Munissy (wa pili kushoto) akikabidhi sehemu ya vyakula vyenye thamani ya shilingi Milioni 1.6 kwa ajili ya mabinti waathirika wa ndoa na mimba za utotoni wanaosoma katika shule ya Sekondari ya Agape Knowledge Open School. Wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Deus Muhoja. Wa kwanza kulia ni Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Bi. Aisha Omary akifuatiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Agape, John Myola na mmoja wa wanafunzi 48 wanaosoma katika shule ya Sekondari ya Agape Knowledge Open School
Sehemu ya vyakula kwa ajili ya mabinti waathirika wa ndoa na mimba za utotoni wanaosoma katika shule ya Sekondari ya Agape Knowledge Open School vilivyotolewa na Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga  
Sehemu ya vyakula kwa ajili ya mabinti waathirika wa ndoa na mimba za utotoni wanaosoma katika shule ya Sekondari ya Agape Knowledge Open School vilivyotolewa na Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga 
Sehemu ya vyakula kwa ajili ya mabinti waathirika wa ndoa na mimba za utotoni wanaosoma katika shule ya Sekondari ya Agape Knowledge Open School vilivyotolewa na Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga 
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe. Nice Munissy (kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Agape AIDS Control Programme (AACP), linalomiliki ya Sekondari ya Agape Knowledge Open School ,John Myola wakati akitembelea Maktaba ya shule hiyo alipowasili kukabidhi vyakula kwa ajili ya wanafunzi wa kike shuleni hapo.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe. Nice Munissy (katikati) akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Agape AIDS Control Programme (AACP), linalomiliki ya Sekondari ya Agape Knowledge Open School ,John Myola wakati akitembelea madarasa ya shule hiyo alipowasili kukabidhi vyakula kwa ajili ya wanafunzi wa kike shuleni hapo.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mhe. Nice Munissy (katikati) akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Agape AIDS Control Programme (AACP), linalomiliki ya Sekondari ya Agape Knowledge Open School ,John Myola wakati akitembelea madarasa ya shule hiyo alipowasili kukabidhi vyakula kwa ajili ya wanafunzi wa kike shuleni hapo.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Post a Comment

0 Comments