Header Ads Widget

JPM ATANGAZA BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI,KATAMBI,GWAJIMA NA CHAMURIHO WATEULIWA

                             
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli

Dar es Salaam. Rais wa Tanzania, John Magufuli leo Jumamosi Desemba 5, 2020 amefanya uteuzi wa mawaziri 21 na naibu mawaziri 23 huku akiwateua waliokuwa makatibu wakuu wa wizara kuwa wabunge na kisha kuwateua kuwa mawaziri.

Pia kiongozi mkuu huyo wa nchi ameanzisha wizara mpya ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na kumteua mbunge wa Kigamboni, Dk Faustine Ndugulile kuwa waziri wa wizara hiyo na Kundo Mathew kuwa naibu waziri.

Akitangaza uteuzi huo katibu mkuu kiongozi, Balozi John Kijazi amesema uteuzi wa mawaziri wawili, Profesa Palamagamba Kabudi (Mambo ya Nje) na Dk Philip Mpango (Fedha) unaendelea na hivyo kufanya idadi ya mawaziri kuwa 23 na naibu mawaziri 23.

Walioteuliwa kuwa wabunge na kisha uwaziri ni Dk Dorothy Gwajima aliyekuwa naibu katibu mkuu Tamisemi akishughulikia sekta ya afya pamoja na Dk Leonard Chamuriho ambaye alikuwa katibu mkuu Wizara ya Uchukuzi.

Majina ya walioteuliwa

Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa- Elias Kwandikwa

Utumishi na Utawala Bora- Kapten John Mkuchika

Wizara ya Ardhi- William Lukuvi

Wizara ya Maji- Juma Aweso

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo- Innocent Bashungwa

Ofisi ya Waziri Mkuu, sera, Bunge, Kazi, Ajira na Wenye Ulemavu- Jenista Mhagama

Wizara ya Afya- Dk Dorothy Gwajima

Ofisi ya Rais Uwekezaji- Profesa Kitila Mkumbo

Wizara ya Katiba na Sheria – Dk Mwigulu Nchemba

Wizara ya Elimu- Profesa Joyce Ndalichako

Wizara ya Mifugo na Uvuvi- Mashimba Ndaki

Wizara ya Maliasili na Utalii- Dk Damas Ndumbaro

Tamisemi- Suleiman Jafo

Wizara ya Nishati- Dk Medard Kalemani

Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi- Dk Leonard Chamuriho

Wizara ya Kilimo- Profesa Adolf Mkenda

Wizara ya Madini- Doto Biteko

Wizara ya Viwanda na Biashara- Godfrey Mwambe

Wizara ya Mambo ya Ndani- George Simbachawene

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (muungano na mazingira)- Ummy Mwalimu

Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari- Dk Faustine Ndugulile

Naibu mawaziri

Wizara ya Viwanda na Biashara- Kigae Silaoneka

Wizara wa Ardhi- Angelina Mabula

Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira- Patrobas Katambi

Wizara ya Mambo ya Ndani- Hamis Hamza Hamisi

Wizara ya Fedha- Mwanaida Ali Khamis

Wizara ya Elimu- Kipanga Juma Omar

Tamisemi- Dk Festo Ndugange

Wizara ya Nishati- Stephen Byabato

Menejimenti Utumishi wa Umma- John Ndejembi

Mawasiliano na Teknolojia ya Habari- Kundo Mathew

Wizara ya Mifugo- Pauline Gekul

Wizara ya Madini- Ndulane Kumba

Wizara ya Ujenzi- Godfrey Kasekenya

Ofisi ya Waziri Mkuu wenye ulemavu- Ummy Ndelinanga

Wizara ya Maji- Maryprisca Mahundi

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo- Abdallah Ulega

Ofisi ya Makamu wa Rais (muungano na mazingira)- Mwita Waitara

Wizara ya Mambo ya Nje- William Olenasha

Wizara ya Maliasili na Utalii- Mary Masanja

Ofisi ya rais Tamisemi- David Silinde

Wizara ya Kilimo- Hussein Bashe

Wizara ya Afya- Dk Godwin Mollel

Wizara ya Katiba na Sheria- Pinda Mizengo

Post a Comment

0 Comments