Header Ads Widget

TANESCO KUONGEZA VITUO VIDOGO VYA KUSAMBAZA UMEME ILI KUWA NISHATI YA UHAKIKA NCHINI

Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi Tanesco(Katikati aliyevaa Miwani)akiwa pamoja na wajumbe wa bodi hiyo pamoja na watendaji wa tanesco Mkoa wa Shinyanga na baadhi wa watumishi wa Tanesco wakiangalia namna utekelezaji unavyoendelea juu ya ukamilishaji wa Kituo hicho eneo la Bulyanhulu Kahama.
Na Kareny Masasi Shinyanga Press Blog 

Mwenyekiti wa  bodi ya Wakurugenzi  wa  Shirika   la Umeme  nchini   (Tanesco)    Dr. Alexander Kiyaruzi amesema kuwa ameridhishwa na hali ya ujenzi wa   kituo kidogo  (substation) kitakachohusika kulisha Mkoa wa Geita uzalishaji wa Umeme kilichopo  Bulyanhulu wilayani Kahama Mkoani Shinyanga  kitachaongeza  nguvu ya kusambaza umeme  katika Mkoa  wa Geita na kupelkea uwepo wa  umeme wa uhakika.

Dakta  Kiyaruzi amesema hayo jana  alipotembelea kituo  hicho kilichopo Bulyanhuru na kusema kuwa uwepo wake utasaidia kuondoa kero ya umeme kutotosheleza mahitaji ya wateja katika Mkoa wa Geita na baadhi ya Maeneo ya wilaya za mkoa wa Kagera na kuwa kukamilika kwake kutaifanya Geita kuwa na umeme mwingi na wa uhakika . 

 “ Umeme utakuwa na nguvu kubwa ya uhakika  unaotoka katika kituo kidogo cha Bulyanhulu  nategemea kitaaanza kazi hivi karibuni ndani ya mwezi huu wa tisa ambapo  lengo la serikali  ni kuhakikisha uwepo wa umeme wa uhakika nchini ikiwezana tuuze nje kwani mahitaji ya Mgodi wa Geita ni Kilovati 30 hivyo itasaidia sana" amesema Dakta Kiyaruzi

  amesema kituo hicho kitaongeza nguvu ya nishati hiyo kwa mikoa hiyo  kwani kitakuwa na kilovati 220 na kupunguza hasara waliyokuwa wakiipata kwa kusafirisha umeme mdogo kutoka  eneo la Ibadakuli lililopo Mjini Shinyanga ambapo ameridhika na maendeleo yake na kuwa ifikapo Septemba 14 umeme utawashwa kwa  ajili ya kuanza kutoa huduma . 

Dakta Kiyaruzi amesema   kutokana na kuwepo kwa viwanda na shughuli za madini  umeme uliokuwepo ulikuwa hautoshelezi mahitaji na kuamua  kuongeza nguvu kwa kujenga kituo  hicho kipya 

“Kutakuwepo na laini nyingine maeneo ya  Nyakanazi itayopelekea Umeme mkoani Kigoma pia Mpanda mkoani Katavi  kwenda Iringa ,Tunduma hadi Sumbawanga na mkoa wa Songwe maeneo hayo umeme utakuwepo wa uhakika lengo ni uhakika wa umeme nchi nzima hivyo watanzania wajiandae tu kwa kukuza uchumi wao kupitia sekta  ya umeme ”amesema  Kiyaruzi.

Kwa upande wake mjumbe wa bodi ya wakurugenzi  Tanesco Dakta John Kihamba  amesema  kuwa Serikali inaboresha miundombinu mbalimbali ikiwemo umeme ili kukuza uchumi  wa   nchi  katika mazingira Mazuri ikiwemo umeme  wa uhakika utakaosaidia kuvutia uwekezaji wa aina mbalimbali ikiwemo viwanda,madini na vinginenvyo 

"Mipango ya Tanesco ni kuhakikisha kwamba kila mwananchi anapata umeme tena umeme wa uhakika kwa hatua amabzo zimefikia hapa umeme kwa mkoa wa Geita kwa sasa upo wa kutosha kwa hiyo yule anayehitaji kuanzisha shughuli zinazotumia umeme watembelee ofisi zetu mahali kokote nchini ili kupata huduma zetu kwani sisi tumejipanga kutoa huduma bora zaidi ya sasa"amesema dakta Kihamba 

Meneja wa mradi huo  Muhandisi James  Masawe amesema  kuwa mradi huo umeanza utekelezaji wake januari 10 ,2019 na unatarajiwa kukamilika septemba 14,2020 ambapo gharama za mradi huo ni  shilingi billion 48.8  ambapo umefikia asimilia 95 katika utekelezaji wake.

"Kwa sasa kazi zinazoendelea ni kufanya majaribio ya mwisho ya mitamo ambayo imefungwa na tunarajia tahehe 14 kuwasha rasmi mitambo hii na kuwapeleka umeme wateja wetu wote katika mkoa wa Geita na wilaya za Mkoa jirani wa kagera ambapo jumla ya vijiji 10 vinapitiwa na Mradi huu ambao utekelezaji wake umefikia asilimia 100 "

Massawe  amesema kuwa wakati wa utekelezaji wa mradi huo wamekumbana na mvua nyingi na kupelekea kupunguza muda wa utendaji pamoja na baadhi ya watalaamu wa ufungaji wa mashine kushindwa kufika kwa wakati kutokana  na zuio la ndege lililosababishwa na uwepo wa ugonjwa wa Covid-19 ambapo kwa sasa wamewasili ili kukamilisha zoezi hilo.

Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Umeme nchini Dk. Alexender Kiyaruzi akipokea maelezo ya mradi huo toka kwa mmoja wa watalaam toka Tanesco wakati wa ziara yao ya kukagua ujenzi wa kituo kidogo kilichopo Bulyanhulu Kahama   
 Ukaguzi wa kituo cha Umeme (Substation)Bulyanhulu ukiendelea 
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Tanesco pamoja na wajumbe wa kamatui hiyo wakiendelea kuangalia namna ambavyo ujenzi huo unavyoendelea katika eneo la Bulyanhulu Kakora Kahama 
  

Juu ni Mojawapo ya nguzo za umeme ambazo zimesimikwa katika kituo hicho.
eneo ambalo lilikuwa likitumika awali na kupokea umeme mdogo ambao ulikuwa haukidhi hitaji la mkoa wa Geita na wateja 
Mitambo Mipya na ya Kisasa ya shirika la umeme iliyopo kwenye kituo hicho cha Bulyanhulu wilayani Kahama ambapo wajumbe wa bodi  na mwenyekti wa bodi wametembelea kuona namna kinavyoendelea na kuridhishwa na ujenzi huo ambao umefikia asilimia 98 
Mfumo wa ndani amabao ni mitambo ya kupokea na kusambaza umeme ikiwa ndani eneo maaalum kwa ajili ya kazi ya kupeleka umeme
Mitambo katika eneo la kituo 
 wajumbe wakiendelea kuangalia mitambo itakayotumika kupeleka umeme Mkoani Geita 
 Wajumbe wakipokea maelezo toka kwa Muhandisi wa mradi huo Bw James Massawe wakati wa