Header Ads Widget

MMILIKI BASI LA HBD, WENZAKE WASHIKILIWA TUHUMA ZA KUCHOMA MOTO BASI HILO



Jeshi la Polisi mkoani Morogoro linawashikilia watu wa tatu akiwemo mmiliki wa Basi la Kampuni ya HBD lenye namba za usajili T 321 DKW, Ahmedi Hemed (25) kwa tuhuma za kuchoma moto basi hilo na kusingizia kuwa limewaka moto baada ya kujam breki.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro amesema kuwa watuhumiwa hao walikula njama ya kufanya tukio hilo baada ya mmiliki kushindwa kulipa deni la basi hilo kwa moja ya taasisi ya kifedha nchini linalodaiwa kufikia zaidi ya milioni 200. Picha na Frank Kaundula.