Na Marco
Maduhu, SHINYANGA
Katibu
Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM Taifa Ally Hapi,
amewataka wana CCM Mkoani Shinyanga, wasibweteke na ushindi ambao wameupata
kwenye uchaguzi mkuu uliopita Oktoba 29 mwaka jana, bali washughulike na
matatizo ya wananchi, kwa kutatua kero zao mbalimbali.
TAZAMA VIDEO👇👇
Amebainisha hayo leo Juni 4,2026 wakati akizungumza na viongozi mbalimbali wa CCM Mkoani Shinyanga kwenye ziara yake ya kuimarisha Chama mkoani humo, pamoja na kuendelea kujenga uhusiano mzuri kati ya CCM na wananchi.
Amesema,
huko mbele kuna kazi kubwa zaidi, bali viongozi wa CCM wanapaswa kufanya kazi
yao ya Chama, kwa kushughulika na matizo ya wananchi, na siyo kutegemea
serikali iwafanyie kazi zao.
“Chama
kikisikia wafanyabiashara wanataharuki lazima wawe wakwanza kwenda eneo la
tukio kusikiliza matatizo yao, sababu wao ndiyo wenye dhamana ya serikali
ambayo ipo madarakani, na kutoa maelekezo ya utatuzi wa kero zao,” amesema
Hapi.
Aidha,
amewataka pia viongozi wanaotokana na dola wakiwamo Wabunge, Madiwani, Wenyeviti
wa Mitaa na vijji, kuhakikisha wanatembelea maeneo yao mara kwa mara, kwa kukagua
utekelezaji wa miradi ya maendeleo, na kusikiliza kero za wananchi na
kuzitatua.
Katika
hatua nyingine amewataka wazazi kuwalea watoto wao katika maadili mema, pamoja
na kusimamia maadili ya vijana, ikiwamo kuwafundisha madarasa ya itikadi.
TAZAMA PICHA👇👇
Katibu wa Jumuiya wa wazazi CCM Taifa Ally Hapi akizungumza.