` KAMATI YA SIASA YA CHAMA CHA MAPINDUZI MKOANI SHINYANGA YAANZA KUFANYA MIKUTANO JUMUISHI KUHAMASISHA UHAI WA CHAMA.

WANDAMAN HOTEL

KAMATI YA SIASA YA CHAMA CHA MAPINDUZI MKOANI SHINYANGA YAANZA KUFANYA MIKUTANO JUMUISHI KUHAMASISHA UHAI WA CHAMA.

 

Kamati ya siasa ya chama cha mapinduzi imeanza utaratibu mpaya wa kufanya mikutano jumuishi inayowahusisha viongozi wa mitaa na mashina nya chama hicho, viongozi wa kata na matawi ya CCM, viongozi na watendaji wa serikali wanachama wa CCM Pamoja na Wananchi kwa ujumla wao lengo likiwa ni kuhakikisha chama kinakua na uhai halisi kwa kusikiliza kero za wananchi na kuzitatua.

Na Mwandishi wetu, Kishapu 

Akizungumza katika mkutano huo jumuishi uliofanyika katika tarafa ya Mondo Wilayani Kishapu, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Bw. Mabala Mlolwa amesema dhamira ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hasan kupitia Chama cha Mapinduzi ni kuhaklikisha kero za wananchi zinatatuliwa sambamba na upatikanaji wa huduma stahiki kwa wakati

Hata hivyo katika mkutano huo wananchi wa Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga wamewasilisha kero zao mbele ya kamati ya Siasa ya CCM ikiongozwa na mwenyekiti Mabala Mlolwa na kati ya kero hizo ni Pamoja na ukosefu wa majisafu na salama katika kata ya seke Bugoro, vyeti vya kuzaliwa kukosekana katyika vituo vya afya na zahanati watoro wanapozaliwa, Changamoto ya kujiandikisha vitambulishio vya Nida Pamoja na Bima ya Afya na kero ya Mnunuzi mmoja wa zao la pamba tofauti na zamani kulipokuwa na soko huria linalojumuisha wanunuzi wengi.

Aidha wananchi hao wamesema kero hizo zimekuwa zikiathiri shughuli zao za uzalishaji mali, huku Afisa Tawala wa Wilaya ya Kishapu Bw.Fadhili Mvanga kwa niaba ya Mkuu wa Wilata hiyo Peter Masindi akieleza kuwa serikali inaendelea kuboresha huduma hizo ili kuwafikia wananchi kwa urahisi zaidi katika maeneo yao ambapo amefafanua kuwa swala la maji ya ziwa Victoria kufikishwa katika kata ya Seke tayari limeshafanyiwa Upembuzi yakinifu na utaratibu unaendelea.

Diwani wa kata ya SekeBugoro Mh. Ferdnand Mpogomi amesema Changamoto kubwa ya kata hiyo ni ubovu wa Miundombinu ya Barabara lakini pia swala la mnunuzi mmoja wa zao la Pamba limekuwa likidhoofisha juhudi za wananchi kulima zao hilo kwakuwa bei ya kilo ya Pamba imekuwa inaporomoka siku baada ya siku kutokana na wanunuzi wanavyojipangia wenyewe.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Mabala Mlolwa amewataka watendaji wa serikali kuhakikisha wanatoa elimu sahihi kwa wananchi namna ya upatikanaji wa huduma mbalimbali kwa kuwasikiliza na kuhakikisha wanatatua  kero wanazoziweza kwa wakati na kero ambazo hawazi kuzitatua wao ka wao wazifikishe sehemi husika ilinazo zitatuliwe mara moja.

Aidha Mwenyekitui wa CCM Mkoa wa Shinyanga Mabala Mlolwa amweataka viongozi wa Chama ngazi zote kuanzia Mkoa hadi mashina kuchukua utaratibu wa vikao na mikutano jumuishi kama nyenzo ya utatuzi wa kero na changamoto zinazoibuliwa na wananchi.






















Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464