

Na Kareny Masasy,
Shinyanga
WADAU Mkoani Shinyanga wametakiwa kushiriki vizuri programu jumuishi ya Taifa ya Malezi Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto (PJT-MMMAM ) pamoja na Mpango Mkakati wa Mkoa wa Kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto (Mtakuwwa) ili kuendelea kujenga jamii kupata kizazi kilichobora.
Hayo yamesemwa leo kwenye kikao cha wadau wa Malezi,Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto kilichofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa kilichoratibiwa na shirika la ICS kwa kushirikiana na Mratibu wa PJT-MMMAM Mkoa ambaye ni Afisa Ustawi wa Jamii Lyidia Kwesigabo .
Kwesigabo akitambulisha MMMAM kwa wadau mbalimbali amesema jukumu kubwa ni kuhakikisha watoto wanakuwa kwa kupata nguzo tano muhimu ambazo ni Malezi yenye mwitikio,Afya bora,Lishe,Ujifunzaji wa Awali na Ulinzi na Usalama na kumuepusha viashiashiria vya hatari ambapo mtoto anakuwa ubongo wake hata kabla ya kuzaliwa.
“Ndiyo maana tumelenga watoto kuanzia umri wa miaka 0 hadi minane na wanapochangamana na watoto wengine kwa kupitia kucheza ,wakubwa kuwapa malezi yenye mwitikio na kuona au kusikia vitu vizuri wanajifunza vitu vingi ambavyo watakuwa navyo na baadaye kuwa watoto wema”.amesema Kwesigabo.
Kwesigabo amesema watoto wasipopata malezi na makuzi bora wanakuwa kwenye hali ya viashiria hatarishi ambavyo wazazi wakiwa wanamigogoro na mtoto anaona,umasikini kutopata lishe bora,kumfungia mtoto ndani asichangamane na watoto wenzake
Ofisa Maendeleo ya Jamii mkoa wa Shinyanga Bestina Gunje akielezea kuhusu mpango mkakati wa taifa unaotokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto ambapo ulianza 2021 hadi 2024 /2025 ambapo mkoa nao ulitoa baadhi ya vipengele vinavyohusu mazingira ya mkoa wa Shinyanga kwa kuangazia mambo nane.
Gunje amesema mambo manane yaliyoainishwa kwenye mpango mkakati wa mkoa ni kuimarisha wananchi kiuchumi,kuondoa ukatili kwenye maeneo ya sokoni, watoto wa kike kupelekwa shuleni.
“Mafanikio yalipatikana kupunguza mimba za utotoni, maeneo ya sokoni kumepungua vitendo vya ukatili ,utolewaji wa mikopo kwenye makundi ya wanawake,vijana na walemavu bila riba na imani potofu zenye madhara zimepungua na sasa wadau wote tujivunie kwenye mafanikio haya” amesema Gunje.
Gunje amesema wamefanikiwa kutoa mafunzo kwa vijana zaidi ya 5000, kugawa taulo za kike kwa mabinti walioko shuleni ili kuhamasisha wasikwame masomo yao, kujenga vituo jumuishi vya wahanga wa ukatili,kupata magari mawili na kuhuisha kamati za Mtakuwwa za kwenye kata.
Gunje amesema mkoa ulioana uhuishe mpango mkakati wa awamu ya pili ulioanza kufanya kazi mwaka 2025/2026 hadi 2030 ambapo katika mambo manane mojawapo kuimarisha uchumi kwenye familia kwa kuendelea kutoa mikopo kwenye makundi maalum isiyo na riba na machinga wote wenye sifa wakope kwenye benk na pia kuwaweka wanaume kwenye mpango huo waweze kueleza nao changamoto zao wanazofanyiwa ukatili.
Kwenye mpango huo tumeingiza mpango mpya ambao haukuwepo ambao ni teknolojia ya habari kukua kwa kasi kubwa ambapo tumetaka matumizi ya teckonolojia iliyopo iwe salama kwa watu wote hata kwa watoto kwani wazazi wamekuwa wakiwaachia simu za mkononi na runinga nakuaacha waangalie bila kufuatilia wanachoangalia.
Lucy Maganga kutoka Shirika la ICS ambalo ni kinara wa utekelezaji wa afua za Malezi na Makuzi ya watoto mkoa na linalofanya uratibu ngazi ya mkoa kwenye jamii na jukumu lao kuu ni kuratibu wadau wote wanaotekeleza shughuli zote za malezi na makuzi ya watoto wadogo ( ECD) kuhakikisha wanaelekea kwenye mrengo mmoja
"Kusaidia uratibu wa watoa huduma ili huduma zinazotolewa na watoto ziwe bora na endelevu nakufanya ushawishi kwa Halmashauri zote sita katika kutenga bajeti ili kuhakikisha watoto wenye umri wa miaka 0 hadi 8 wanapewa huduma stahiki na kuwataka wadau wote wanaofanya huduma za watoto kujiunga na mtandao wa Malezi (Tecden) ili kutekeleza vyema shughuli zao"amesema Maganga.
MWISHO.

Mratibu wa PJT-MMMAM Mkoa ambaye ni Afisa Ustawi wa Jamii Lyidia Kwesigabo .

Lucy Maganga,Mwakilishi wa Shirika la Invest in Children Society (ICS) linaloratibu shughuli za malezi na makuzi-mkoa wa Shinyanga

.jpeg)

.jpeg)
Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464
