` RAIS SAMIA AMUASILI MTOTO ALIYETELEKEZWA TABORA

WANDAMAN HOTEL

RAIS SAMIA AMUASILI MTOTO ALIYETELEKEZWA TABORA


Picha: Ikulu

Rais Samia Suluhu Hassan, akiwa amembeba mtoto aliyemuasili.

Rais Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto mchanga wa kike aliyepewa jina la Grace Samia Suluhu katika makazi yake ya Ikulu Chamwino mkoani Dodoma leo, Machi 11, 2026.

Mtoto huyo alitelekezwa awali katika mji wa Nzega mkoani Tabora na baadaye kukabidhiwa kwa Rais na Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Naitapwaki Tukai.

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Wilaya, mtoto huyo aliokotwa Januari 17, 2026 karibu na nyumba ya wageni ya Kasulu, Nzega Mjini. Baada ya kupatikana, alichukuliwa kwa ushirikiano na Jeshi la Polisi Tanzania na kupelekwa hospitalini kwa uchunguzi, huku juhudi za kumtafuta mama yake zikiendelea bila mafanikio.

SOMA ZAIDI HAPA CHANZO NIPASHE.


Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464