
Hakimu mkazi mfawidhi mahakama ya
Wilaya ya Shinyanga Yusuph Zahoro kwa mujibu wa kifungu cha sheria namba
130(2)(e) ametoa hukumu hiyo baada ya kusoma mwenendo wa kesikwa hiyo leo
Novemba 12, 2025 katika Mahakama ya wilaya ya Shinyanga amesema kuwa kwa mujibu
wa mlalamikaji ambaye ni shahidi wa kwanza, aliibiwa simu na mshtakiwa akiwa na
mwenzie maeneo ya Ngokolo mitumbani na katika kuifuatilia mshtakiwa akamtaka
aifuate simu hiyo maeneo ya Tambukareli alipofika ndio alipoingiliwa na wanaume
hao wawili, mmoja baada ya mwingine.
Aidha hakimu Yusuph Zahoro amesema Kifungu
hicho cha sheria namba 130(2)(e) mtu atahesabiwa ametenda kosa la kubaka endapo
atafanya tendo la ndoa na mtoto wa kike mwenye umri wa chini ya miaka 18 iwe
kwa ridhaa au bila ridhaa yake, kifungu cha 131(1) kinaeleza adhabu mtu yeyote
atakayepatikana na hatia ya kubaka atahukumiwa kifungo cha maisha jela ili iwe
funzo kwa watu
Naye Wakili wa serikali Katandukila
Kadata kutoka Mahakama ya wilaya ya Shinyanga amesema kuwa kutokana na kosa
hilo na ushahidi ulipo mshtakiwa apewe adhabu kali ili iwe funzo kwa vijana
wengine,
Hata hivyo mshtakiwa Bw. Mackighty
Julius alipotakiwa kujieleza kwanini asihukumiwe na kupewa adhabu kali amejaribu
kujitetea na kumuomba hakimu ampunguzie kwa madai kuwa ana watoto wadogo na mke
pamoja na mama yake mzazi ambaye ni mjane kufuatia Baba yake mzazi kufariki
dunia.
“Mheshimiwa
naomba kupunguziwa adhabu kwani nina familia ya mtoto, mke, mama mzazi pia na
bibi yangu wote wananitegemea, mimi ndio kila kitu baba yangu alishafariki na
wadogo zangu pia wananitegemea katika matumizi ya nyumbani na shuleni, ‘Naomba
nisamehewe mheshimiwa’” amesema Mackighty Julius.
Na kisha hakimu wa Mahakama ya
Wilaya ya Shinyanga Yusuph Zahoro kwa kwa kizingatia kifungu hicho cha sheria namba
130(20(e) amesema mahakama imemtia hatiani Bw. Mackighty Julius (21) mkazi wa Manispaa ya
Shinyanga kifungo cha maisha jela ili iwe fundisho kwa watu wengeine wenye
tabia kama hizo.