` NSSF TUNAENDELEA KUTOA ELIMU YA HIFADHI YA JAMII: KARIBU TUKUHUDUMIE

NSSF TUNAENDELEA KUTOA ELIMU YA HIFADHI YA JAMII: KARIBU TUKUHUDUMIE

 

Wananchi mbalimbali wakiendelea kupata elimu ya hifadhi ya jamii katika banda la NSSF wakati wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali, jijini Dodoma.

NSSF inashiriki maonesho haya kwa lengo la kutoa elimu ya hifadhi ya jamii kwa ujumla ikiwemo elimu kuhusu mafao, jinsi ya kujisajili kwa wanachama wapya kutoka sekta binafsi na wananchi waliojiri wenyewe, pia wanapewa elimu jinsi wanavyoweza kujichangia kupitia simu ya mkononi popote walipo, fursa za uwekezaji katika miradi ya nyumba na viwanja na elimu kuhusu huduma za kidijiti (NSSF Portal).


Kama una Taarifa, Habari, Tangazo n.k Wasiliana nasi kupitia shinyapress@gmail.com au +255 788 469 464