Hizi fedha nyingi ambazo nimekuwa nazipata naweka benki”
Wanasema katika maisha kama hujabahatika kwenda shule na kupata elimu usichague kazi, kwani mchagua jembe si mkulima. Walisema waswahili. Usemi huo umekuwa ukiishi katika maisha yangu miaka yote.

Naitwa Baro, kijana wa miaka 23, sikufanikiwa hata kumaliza elimu ya msingi kwani niliishia darasa la nne, hiyo ni baada ya wazazi wangu kutengana hivyo nikaenda kuishi na bibi yangu na huko maisha yalikuwa magumu sana kiasi kwamba nikashindwa kuendelea na masomo