Header Ads Widget

MANISPAA YA SHINYANGA KUHAMASISHA VIJANA KUJIUNGA CHUO CHA MATANDA VTC

 MANISPAA YA SHINYANGA KUHAMASISHA VIJANA KUJIUNGA CHUO CHA MATANDA VTC

Na mwandishi wetu.

Halmashauri ya manispaa ya Shinyanga  imeahidi kuweka mikakati ya kuhamasisha vijana wa manispaa ya Shinyanga kujiunga na Chuo cha matanda VTC  ili kuweza kupata mafunzo ya  fani za ushonaji, ufundi wa magari,umeme na udereva  ili

kukabiliana na tatizo la ajira kwa vijana.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa kamati ya  afya,elimu na uchumi ya manispaa ya Shinyanga, ambaye  pia ni diwani wa kata ya Lubaga,Reuben Masanja wakati akifungua mahali ya tatu ya chuo cha matanda vtc  leo novemba 17,2023 kwa niaba ya meya wa manispaa ya Shinyanga,

Kauli hiyo ameitoa  kutokana na vijana  wa manispaa ya Shinyanga  kutokuwa  miongoni  mwa wahitimu wa  kozi hizo kwa mwaka  huu   na  wengi kukosa fursa za ajira kutokana na kutokuwa na ujuzi ili kukabiliana na mahitaji ya soko la ajira.

Reuben anasema,anasikitishwa kwa kutoona hakuna hata kijana moja anayetoka manispaa ya Shinyanga aliyehitimu mafunzo kutoka chuo hicho licha ya kuwa kipo ndani ya manispaa.Vijana wengi waliohitimu katika chuo hicho wametoka mikoa ya mbali na halmashauri zingine ndani ya mkoa wa Shinyanga.

Reuben alisitiza uongozi wa chuo hicho kuweka jitihada zaidi za kujitangaza ili kutoa fursa kwa wana jamii kuweza kupeleka watoto wao katika chuo hicho ili kusaidia vijana kupata ajira kadri ya kozi zinazotolewa na chuo hicho.

Mwenyekiti wa kamati ya  afya,elimu na uchumi ya manispaa ya Shinyanga, ambaye  pia ni diwani wa kata ya Lubaga,Reuben Masanja akizungumza katika mahafali ya chuo cha matanda VTC.

"Hatuna budi,manispaa kutumia majukwa yetu kufanya kampeni ya matangazo zaidi ili vijana wajiunge na chuo hiki kwa ajili ya kozi zinazotolewa kwani kuna mambo mazuri na jamii haifahamu uzuri wa chuo cha matanda,ni masikitiko kwa kuwa vijana wengi wanatoka mikoa ya mbali na vijana wetu hawachangamkii fursa hii" anasema Reuben.

 "Naombeni uongozi wa chuo kwa nafasi yenu kufanya matangazo zaidi katika nyumba za ibada ili vijana waweze kutambua fursa hii kwani ada yenu ni Shs 600,000 kwa mwaka ,ambayo hata kaya maskini  zinaweza kuimudu."anasema Reuben.

 "Pia tunalichukua suala hili la kuweza kufadhili wanafunzi wa kike 17 kutoka manispaa ya Shinyanga ili wapate ujuzi katika chuo hiki" anasema Reuben.

Kwa upande wake, Mkuu wa chuo cha matanda,Joaster Thomas Kisanko aliomba,Halmashauri hiyo kuweza kufadhili wasicha 17 kutoka kata za manispaa ya Shinyanga ili kusaidia wasichana katika kujikuwamua kiuchumi na kutoa wito kwa wazazi na walezi kupeleka watoto chuoni hapo. 

"Ni wakati muhimu wa kuleta vijana katika chuoni kwa kuwa ziko fursa za ajira  kwa maeneo mbalimbali baada ya kuhitimu kozi zinazotolewa na chuo chetu na tunaomba Halmashauri  ya manispaa  ya Shinyanga kufadhili wasichana 17 pekee kutoka katika kata zao ili tuwapatie mafunzo ya kuweza kujiinua kiuchumi kwa maisha ya badaye"anasema Kisanko

Aidha ,Mkurugenzi wa Central Link logistic Tanzania, Wiliam James ,anasema wameamua kushirikiana na chuo kwa kutoa mafunzo ya umeme na kuwatumia vijana hao katika miradi ya REA kwa kushirikiana na Tanesco.

Mkurugenzi wa Central Link logistic Tanzania, Wiliam James akizungumza kuhusu ushirikiano wa mafunzo ya umeme wanayotoa katika chuo cha matanda VTC.

" Vi vema vijana kupata ujuzi ili kuweza kupata fursa ya ajira ,hiki ni chuo cha pili Tanzania kukipatia mafunzo na hata Tanesco mkoa wa Shinyanga  walifurahi kuona ujio wetu kwa kuwaanda vijana kwa ajili miradi ya umeme"anasema william

Mratibu wa mafunzo chuo cha matanda VTC, Malia Elisapetha akizungumza na kutoa shukrani kwa wahitimu wote.

Nao baadhi wanafunzi waliohitimu chuo hicho walisema wataweza kuendesha maisha yao na kujenga uchumi wa nchi baada ya kuhitimu mafunzo kwa miaka miwili kwa yale waliojifunza.

 " Tunaomba serikali  ikishike mkono chuo hiki ili kusaidia vijana wengine kuweza kupata mafunzo yatakayosaidia kupata ajira na tuna ahidi kulitumikia Taifa na kuijenga nchi yetu" anasema Ramadhan Said.

 "Napenda sana ushonaji na nimejifunza hapa kwa miaka 02 na nitakwenda kuendelea na kazi hii huko mitaani"anasema Diana Kija:

 "Niko tayari kutoa huduma za ufundi wa magari baada ya  kupata ujuzi  huu kwa miaka miwili kwa kile nilichojifunza hapa"anasema Ernest Stanslau.

Wahitimu wa chuo cha matanda VTC wakionesha ujuzi kwa fani zao
Centre link logistic wakionesha fursa za miradi ya umeme Tanzania kwa makapuni mbalimbali.
Wahitimu wa chuo cha matanda VTC wakiingia katika ukumbi
Viongozi wa matanda VTC na wanafunzi wakicheza.

Mgeni rasm akitoa vyeti kwa wahitimu chuo cha matanda  VTC




Post a Comment

0 Comments