Header Ads Widget

YANGA WAIFANYA MBAYA SIMBA SC KWA MKAPA!! WAIDUNGUA 5- 1

 


Dakika 90 za Mchezo wa Kariakoo Dabi Uwanja wa Mkapa Jijini Dar es salaam zimemalizika kwa shangwe kubwa kwa Yanga SC na kilio kizito kwa Simba SC!!! Yanga SC wameichakaza Simba SC Bao 5 - 1.

Kipindi cha pili Yanga walionyesha wanahitaji ushindi na kufunga mabao kupitia kwa Maxi Nzengeli ambaye alifunga mawili dakika ya 64, 77, Aziz KI dakika ya 73, Pacome bao la tano dakika ya 87 kwa mkwaju wa penalti.

Dakika 45 za mwanzo ubao umesoma Simba 1-1 Yanga.

Bao la Yanga lilifungwa dakika ya tatu na Kennedy Musonda na bao la Simba limefungwa na Kibu Dennis dakika ya 8.

Post a Comment

0 Comments