Header Ads Widget

JKT-TANZANIA,KAGERA SUGAR WATOSHANA NGUVU UWANJA WA CCM KAMBARAGE MJINI SHINYANGA


KT-TANZANIA, KAGERA SUGAR WATOSHANA NGUVU UWANJA WA CCM KAMBARAGE MJINI SHINYANGA

Na Mwandishi wetu 

Timu ya JKT Tanzania wametoka thuruhu ya goli 1 - 1 dhidi ya Kagera Sugar kwenye nmchezo wa ligi kuu NBC Tanzania Bara.


Mchezo huo uliochezwa leo Septemba 29, 2023 katika uwanjan wa CCM Kambarage Mjini Shinyanga uliomalizika kwa droo ya goli 1 - 1 huku magoli yote yakifungwa dakika za nyongeza goli la JKT Tanzania likifungwa na Daniel Lyanga kwa mkwaju wa penati Dk 97 huki goli la Kagera Sugar likifungwa na Gasper Mwaipasi Dk 98.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo kocha msaidizi wa timu ya JKT Tanzania George Mketo amesema makosa waliyofanya baada ya kupata goli ndio limewaadhibu na kupelekea wapinzani wao kupata goli na kufanikiwa kusawazisha.

Kwa upande wake kocha msaidizi wa timu ya Kagera Sugar Marwa Chambeli amewapongeza wachezaji wake kwa kupambana na kufanikiwa kusawazisha goli na kugawana pointi kwenye mchezo huo.

Post a Comment

0 Comments