Header Ads Widget

BAADHI YA WAZAZI NA WALEZI WA KATA YA MWAKITOLYO KUZUIA WATOTO KUPATA ELIMU

 

BAADHI YA WAZAZI NA WALEZI WA KATA YA MWAKITOLYO KUZUIA WATOTO KUPATA ELIMU

Frank Medembo, Mwalimu Mkuu Msaidizi katika shule ya Msingi Mwakitolyo akizungumza na SPC blog.

 Zubeda Mohamed wa darasa la tatu shule ya msingi Mwakitolyo akizungmza na SPC blog.

Baadhi ya wanafunzi wa shule ya  msingi Mwakitolyo wakifurahia kutembelewa na shinyanga press club blog kupaza sauti zao juu ya ukatili wa kijinsia.

Na Mwandishi wetu.

Waalimu wa  shule za msingi katika kata ya Mwakitolyo wamelalamikia baadhi ya wazazi na walezi  kuwanyima haki ya msingi ya elimu watoto wao kwa kuwatumikisha kwenye shughuli mbalimbali za  familia  bila kutambua umuhimu wa elimu.

Waalimu hao wa kata ya Mwakitolyo wameieleza Shinyanga Press Club blog ilipotembelea kata ya Mwakitolyo ikiwa na lengo la kungalia hali ya vitendo vya  ukatili dhidi ya wanawake na watoto ndani ya eneo hilo.

Baadhi ya wazazi na walezi ndani ya Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga wamekuwa na vitendo vya kuwanyima watoto wao haki ya elimu kwa kuwatumikisha shughuli za ufugaji,kilimo,madini na kulea watoto.Aidha uelewa mdogo, mila na desturi imeelezwa kuwa chanzo cha kuwanyima watoto haki ya elimu.

Frank Medembo, Mwalimu Mkuu Msaidizi katika shule ya Msingi Mwakitolyo anasema kuwa wazazi wamekuwa wakitumia sababu zisizo na mashiko za kuomba ruhusa ili kwenda kuwatumikisha watoto katika shughuli mbalimbali.

 “Mzazi  anaomba kuhusa inayohusu msiba wa mtu ambao hawahusiani ili akae na mtoto wiki moja hadi wiki mbili,lakini pia watoto wengine hawaji shule kwa sababu za kiuchumi kwa wazazi kuwacha nyumbani na kisha  wazazi kwenda shamba,wapo baadhi ya wanafunzi wameacha shule na ukiuliza wenzao,wanakuambia wapo kwenye marambo”Alisema Frank

Pia mwalimu Zubeda Mohamed wa darasa la tatu shule ya msingi Mwakitolyo alisema,wazazi kufika shuleni na kuomba ruhusa ya watoto wao wabaki majumbani ili wao waende gulio au mke wangu amejifungua hivyo mtoto akasaidie mama yake kazi.

“Uchimbaji ni chamgamoto kubwa sana kwa sababu kuna vishawishi vingi kwa watoto wa kike kwa kukutana na wavulana ambao wako katika uchimbaji na kusababisha mimba na kuacha shule” Alisema Zubeda.

Dina Pius mwanafunzi wa darasa la sita wa shule ya msingi  Mwakitolyo,alieza kuwa wazazi na walezi kuwafanyia ukatili watoto wenzake  kwa kuwanyima kufika shule na kuwapa kazi majumbani.

 Aina za ukatili wanaofanyiwa watoto ni utoro shuleni, kufanyishwa kazi, kuponda mawe,kufanya kazi za hotelini na maduarani ili watafute hela”Alisema Dina

Naye mtendaji wa kata ya Mwakitolyo,Lutemba Butonja alisema,Watoto wengi wanajua wakienda kuchimba wanapata fedha na hivyo wanaamini wakisoma hawawezi kupata fedha,ambapo anasema kuwa suala hilo limedhibitiwa.

“Tumejitajidi sana kuthibiti hili kwa kuhakikisha kwamba tunafata sheria ya kutumikisha watoto ,tusimwone chini ya miaka 18 mtoto anafanya kazi na shughuli za uchimbaji,kama serikali tumekuwa tukisimamia sana na kuwapa elimu kwa wale watu wanao ajiri watoto kwa kufata sheria kuwa hairuhisiwi kuajiri mtoto chini ya miaka 18 na hii imetusaidia sana”

 


Post a Comment

0 Comments