Header Ads Widget

TRA -KAHAMA YAWASHUKURU WAFANYABIASHARA YAVUKA LENGO KWA USHIRIKIANO.



MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa kikodi Kahama  wakiwa katika kilele cha maadhimisho ya siku ya  shukrani kwa mlipa kodi  pamoja na baadhi ya wafanyabiashara.

Na  Kareny  Masasy, Kahama

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa kodi Kahama  umejivunia kuvuka lengo kwenye ukusanyaji wa mapato kwa kipindi  kuanzia mwezi Julai hadi  Oktoba mwaka 2022.

Meneja  mkoa wa kikodi Kahama Warioba Kanile amesema hayo leo tarehe 28/Novemba/2022  katika kilele cha maadhimisho ya shukrani kwa mlipa kodi yaliyohudhuliwa na wafanyabiashara huku mgeni rasmi akiwa mkuu wa wilaya ya Kahama Festo  Kiswaga.

Warioba amesema maadhimisho hayo yamekwenda na ujumbe unaosema “Asante kwa kulipa kodi kwa ustawi wa  jamii  na maendeleo ya Taifa -kazi iendelee” ikiwa makusanyo kwa kipindi hicho  walipangiwa lengo zaidi ya sh Billioni 5.9 na  makusanyo yakawa zaidi y ash Billioni 7.1 ambayo ni ufanisi wa asilimia 119.71.

“Lengo la  maadhimisho haya ni kutambua mchango na ushirikiano  uliopo baina ya TRA na wadau wake  na kupitia maadhimisho  imekuwa ikiwaweka pamoja  na wadau  kwa kushiriki  katika shughuli mbalimbali  za kijamii,burudani  na kupata mrejesho”amesema Kanile..

Mwakilishi wa kamishna mkuu kutoka makao makuu TRA  Ndositwe  Haonga amesema Siku ya mlipa kodi ni siku iliyotengwa rasmi  kwaajili ya kutambua  mchango inayotolewa  na walipakodi katika ngazi zote hivyo inawahusu wananchi wote.

Haonga amesema dhamira  ya siku ya mlipakodi ikiwa ni ileile kwa kuamini kwamba kuna usimamizi mzuri wa kodi ndani ya nchi .

 Haonga amesema ipo  tija na ufanisi wa hali ya juu kwa ushirikishwaji   pamoja na kuchukua mawazo na mapendekezo ya mlipa kodi katika kutunga sheria na sera za kodi,kujadiliana juu ya mbinu na mikakati mbalimbali.

“Tunapowaenzi walipakodi tunatambua kuwa hadhi yao imetoa mchango mkubwa katika kulinda uhuru wa taifa  pia  kutambua  wanaofanya vizuri  inakuwa ni moja ya motisha muhimu ya kuendeleza ufanisi”amesema Haonga..

Haonga amesema wanafahamu wapo walipakodi wachache ambao wana ridhaa ndogo ya kulipa kodi na  wale ambao hawalipi kabisa kodi  ambayo ni stahiki ya serikali  wanatakiwa kubadilika na kuiga mfano.

“Katika kutimiza hili TRA imedhamiria  kuongeza ukusanyaji wa mapato kwa kuimarisha  namna ya ukusanyaji,udhibiti wa mianya  ya upotevu wa kodi,kubainisha  vyanzo vipya vya mapato na kuweka mazingira rafiki kwa walipakodi nakuwa na mifumo ya usimamizi wa kodi ili kurahisisha ulipaji kodi”amesema Haonga.

Mkuu wa wilaya ya Kahama Festo Kiswaga amewapongeza  TRA kwa kutomuangusha  kutokana na ukusanyaji mzuri wa mapato, ila bado kuna changamoto ya  wafanyabishara kutotoa risti  kwani anawashauri wakitoa risiti hata mteja hasumbuliwi na kuweka kumbukumbu zao vizuri katika biashara.

“Wafanyabiashara wapatiwe elimu mara kwa mara  na wachangie kimawazo  walio wengi hawana elimu na mashine za Kielektroniki (EFD) hakuna budi kwenda na mabadiliko ya sasa  mashine  hizo zitaondoa changamoto zote walizonazo”.amesema Kiswaga.

Kiswaga amekabidhi vyeti vya utambuzi wa walipakodi katika makundi  ya wafanyabiashara wadogo,wakati na wakubwa ambapo zawadi ya ushindi wa jumla ilikwenda kwenye shirika la PANAFRICAN MINING SERVICES LTD

Mwenyekiti wa chemba ya biashara,viwanda na kilimo (TCCIA)  Charles Machali amesema  hivi sasa kuna uhai kati ya wafanyabiashara na TRA  na ndiyo maana unaona biashara za  ufunguzi wa maduka zimeongezeka  wanachohitaji ni kupatiwa elimu zaidi.


Upande wa kushoto ni  meneja kutoka mamlaka ya Mapato Tanzania mkoa wa kikodi Kahama  Warioba Kanile akiwa na mwakilishi wa kamishna mkuu kutoka makao makuu  Ndositwe Haonga.

Wadau wakiwa kwenye ukumbi wakisikiliza  hotuba za mamlaka ya mapato TRA  zikitolewa na  maafisa wa mamlaka hiyo.

Kamti ya ulizi na usalama ya wilaya ya Kahama 

Mkuu wa wilaya ya Kahama Festo Kiswaga akimpatia cheti   mmiliki wa shule za Rocken Hill na Anderleck  alichopewa na TRA.

Mkuu wa wilaya Festo Kiswaga akiendelea kutoa vyeti kwa  wafanyabiashara.


Mkuu wa wilaya ya Kahama Festo Kiswaga naye akikabidhiwa cheti kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa kikodi Kahama  na mstahiki meya wa manispaa ya Kahama Yahya Bundala.

Wafanyabiashara wakisikiliza 

Mwenyekiti wa TCCIA wilayani Kahama Charles Machali

Post a Comment

0 Comments