Header Ads Widget

MADIWANI SHINYANGA WAMUUNGA MKONO RAIS SAMIA KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII, DC MBONEKO APONGEZA FILAM YA THE ROYAL TOUR

Tembo akiwa katika hifadhi Mbuga ya wanyama Serengeti.

Na Marco Maduhu, SERENGETI

MADIWANI wa halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, wakiambatana na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, pamoja na watumishi, na viongozi wa CCM, wametembelea hifadhi ya Mbuga za wanyama Serengeti, ili kuunga mkono kujuhudi za Rais Samia kutangaza vivutio vya utalii hapa nchini.

Ziara hiyo imeanza leo Novemba 11,2022 kwa kutembelea hifadhi ya Mbuga za wanyama Serengeti, ambapo kesho Novemba 12 watatembelea Mbuga za wanyama Ngorongoro.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, akizungumza kwenye ziara hiyo ya kuhamasisha utalii, amesema wameamua kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kutangaza vivutio vya utalii hapa nchini na kuongeza pato la taifa.

"Unapohamasisha vivutio vya utalii, ni vyema wewe Mtanzania uvitembelee pia, ili kuunga juhudi za Rais Samia kutangaza vivutio vya utalii, ndicho tulichokifanya sisi kutembelea Mbuga za wanyama,"amesema Mboneko.

"Tunampongeza Rais Samia kwa Filam ya The Royal Tour ambayo imetangaza vivutio vya utalii hapa nchini, na leo tumeshuhudia hapa Serengeti mamia ya watalii kutoka nchi za kigeni wakimiminika kutalii," ameongeza.

Aidha, ametoa wito kwa watanzania kujenga utamaduni wa kutembelea vivutio vya utalii hapa nchini, zikiwamo mbuga za wanyama ili kujifunza mambo mengi na kuchangia pato la taifa.

Nao baadhi ya madiwani akiwamo Zamda Shambani, amesema ni mara yake ya kwanza kutembelea Mbuga za wanyama, na amejifunza mambo mengi pamoja na kuona wanyama live wakiwamo Tembo, Twiga, Pundamilia pamoja na Simba.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akizungumzia ziara hiyo ya utalii katika hifadhi Mbuga ya wanyama Serengeti.

Diwani wa Ndala Zamda Shabani akizungumza katika ziara hiyo ya utalii kwenye Mbuga ya wanyama Serengeti.

Diwani wa Mwawaza Juma Nkwabi akizungumza katika ziara hiyo ya kuhamasisha utalii.

Diwani wa Ibinzamata Ezekiel Sabo akizumgumza katika ziara hiyo ya kuhamasisha utalii.

Madiwani wa Manispaa ya Shinyanga wakiwa ziara katika Mbuga ya wanyama Serengeti kuhamasisha utalii.

Madiwani na watumishi wa halmashauri ya manispaa ya Shinyanga wakiangalia wanyama katika Mbuga ya wanyama Serengeti.
Uangaliaji wanyama ukiendelea katika Mbuga ya Serengeti.

Uangaliaji wanyama ukiendelea katika Mbuga ya Serengeti.

Uangaliaji wanyama ukiendelea katika Mbuga ya Serengeti.

Uangaliaji wanyama ukiendelea katika Mbuga ya Serengeti.

Uangaliaji wanyama ukiendelea katika Mbuga ya Serengeti.

Uangaliaji wanyama ukiendelea katika Mbuga ya Serengeti.
Uangaliaji wanyama ukiendelea katika Mbuga ya Serengeti.

Uangaliaji wanyama ukiendelea katika Mbuga ya Serengeti.

Uangaliaji wanyama ukiendelea katika Mbuga ya Serengeti.
Uangaliaji wanyama ukiendelea katika Mbuga ya Serengeti.

Uangaliaji wanyama ukiendelea katika Mbuga ya Serengeti.

Tembo akiwa katika hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.

Pundamlia akiwa katika hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.
Simba wakiwa katika hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.
Wanyama wakiwa katika hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.
Wanyama wakiwa katika hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.
Wanyama wakiwa katika hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.
Wanyama wakiwa katika hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.
Simba wakiwa katika hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.
Twiga wakiwa katika hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti
Wanyama wakiwa katika hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.

Wanyama wakiwa katika hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.

Wanyama wakiwa katika hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.

Wanyama wakiwa katika hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.

Wanyama wakiwa katika hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.

Wanyama wakiwa katika hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.

Mamba akiwa katika mto ndani ya hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.
 
 viboko wakiwa ndani ya maji kwenye hifadhi ya wanyama Serengeti.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko akipiga picha kwenye kibao cha hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.

Mwandishi wa habari Franki Mshana akipiga picha katika kibao cha hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.

Picha za pamoja zikipigwa kwenye kibao cha hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.

Picha za pamoja zikipigwa kwenye kibao cha hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.

Picha za pamoja zikipigwa kwenye kibao cha hifadhi ya Mbuga ya wanyama Serengeti.

Post a Comment

0 Comments