Header Ads Widget

ASASI ZA KIRAIA ZIFANYE UTAFITI KATIKA MILA & DESTURI KUFANIKISHA HARAKATI ZA UFEMINISTI

ASASI ZA KIRAIA ZIFANYE UTAFITI KATIKA MILA & DESTURI KUFANIKISHA HARAKATI ZA UFEMINISTI.

Rebecca Mjema Kisenha Mwezeshaji wa wa masuala ya ufeministi.

Na Mwandishi wetu.

Asasi za kiraia zinazopamba na kutomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto mkoa wa Shinyanga zimeshauriwa kufanya utafiti zaidi katika kuweza kuboresha mikakati na mipango ya ufeministi ili  kuwakomboa wanawake wa pembezoni.

Hayo yameelezwa leo jumatano 16,Novemba,2022 na Rebecca  Mjema ambaye ni mwezeshaji wa mafunzo y ya ufeministi yaliyofanyika katika hoteli ya Karena Manispaa ya Shinyanga,ambapo asasi za kirai zipatazo 28 za mkoa wa Shinyanga zimeshiriki mafunzo hayo.

Rebeca Alisema,Ni wakati wa wadau kuvaa uhalisia wa maisha halisi ya wanawake na watoto wa pembezoni kwa kufanya utafiti wa mila na desturi za walengwa.

" Mila na desturi ni zimebeba dhamana kubwa ya walengwa na ndani ya jamii  zipo mila na desturi ambazo ni mbaya na nzuri,Hivyo wajibu wetu kuzifanyia kazi zile ambazo ni mbaya zinazo wakandamiza wanawake na watoto.Alisema Rebecaa.

" TAPO lenu  la SHY-EVAWC kila moja ana rasilimali kwa shirika lake  katika kuweka umoja wenye nguvu wa kuweza kuwa na mbinu na mipango bora na imara kwa kuweza kuwakomboa wanawake na watoto dhidi ya ukatili"

Naye,Charles Deogratius wa shirika la WAYDS alisema ni mila na desturi zimekuwa zinabadilika ni wakati wa kuzitambua ili kuweza kuwa na utekelezaji rahisi wa shughuli zetu.

Washiriki wa mafunzo ya nguvu ya TAPO na ufeministi wakiwa katika shughuli za vikundi.
Wawakilishi kutoka kazi za makundi wakiwasilsha shughuli za kazi za vikundi.
Waratibu wa mafunzo ya ufeministi na nguvu ya TAPO wakifatilia na kuchukua kumbukumbu za mafunzo.
Mpangilio wa kumbukumbu za mafunzo ya nguvu ya TAPO na ufeministi.

Post a Comment

0 Comments